Weka Email Yako Hapa Upokee Makala Kama Hizi

Kwenye maisha yetu ya kila siku kuna mambo mengi hutokea na kwa namna moja au nyingine mambo haya yanatuathiri moja kwa moja au kwa sehemu. Kila siku kuna mtu atakuwa amezidiwa na akakimbizwa hospitali, kuna ambaye atafiwa, kuna ambaye atapata ajali, kuna ambaye ataibiwa, kuna ambaye atapoteza pesa, kuna ambaye atafanya uzembe Fulani, na mengine mengi sana.

Haya ni mambo yanayotokea katika maisha yetu ya kila siku. Kwa bahati mbaya sana haya mambo mengi hatuna uwezo wa kuyathibiti. Huwezi kuzuia mtu mwingine asiwe mgonjwa asiibiwe, asipate ajali, na hivyo basi yanapotokea yanakuwa ni mambo ambayo tusiyoyatarajia.

Leo natamani kuona wewe unakuwa mtu mwenye furaha na maisha yako yanakuwa bora lakini bado haya mambo yatakuwa yanaingilia furaha yako ya kila siku, mipango yako binafsi,  na hata yale mambo ya muhimu.

Inawezekana wewe ni dereva mzuri sana, hujawahi kupata ajali, hujawahi kuandikiwa kosa lolote hata la bahati mbaya na askari wa usalama barabarani. Siku moja asubuhi unaamka ukiwa na mipango yako mizuri sana, unaingia barabarani halafu unajikuta upo kwenye foleni ambayo itakuchelewesha labda kwa masaa kadhaa. Foleni ile imesababishwa na dereva moja mzembe ambaye amepata ajali. Akaathiri ratiba zako zote za siku nzima. Ubora wako kwenye udereva hapo hautakusaidia chochote.

Unachotakiwa kwenye maisha yako ya kila siku, ni kujiandaa kwa yale ambayo hayatarajiki. Hakuna anaemka asubuhi na kutarajia kwenda kupata ajali, au kuibiwa, au hata kuumwa. Kila mmoja anatarajiwa mambo mazuri. Lakini mambo mabaya hayaachikuja. Yanakuja kwasababu ndio asili ya dunia. Kila saa kuna mambo mengi yanaendelea na yanaweza kukuathiri wewe moja kwa moja au kwa sehemu.

Unachopaswa kuelewa ni kutarajia yasiyotarajiwa. Unapanga mambo yako lakini unaweka akili kwamba lolote pia linaweza kutokea likasababisha hii mipango yako ikakwama. Wakati mwingine sio lazima ujiandae na mabaya, lakini unapaswa tu kuelewa yanaweza kutokea popote na yakakukuta bila kujalisha wewe ni mwadilifu kiasi gani. Ukiwa na hili kichwani mwako hata itokee nini huwezi kuumizwa sawasawa na Yule ambaye akili yake aliiweka kwenye upande mmoja pekee. Kama vile anaishi peke yake hapa duniani.

UNAPOTARAJIA MAMBO MAZURI MAKUBWA KWENYE MAISHA YAKO USIACHE PIA KUTARAJIA NA YASIYOTARAJIWA.

Ni mimi rafiki Yako wa Siku Zote Jacob Mushi.

One Response

Leave a Reply to BARAKA UZIMACancel reply

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading