Category Archives: USHAURI

512; Mimi Ni Mtenda Dhambi Kuliko Wewe.

Siku Moja nilikuwa nawaza hivi, “Siku Nikifa Nikakuta hakuna Mungu Nitacheka Sana”, Sauti nyingine ndani yako Ikasema, “Hapo Utakapokuwa Unachekea ni Nani Huyo Atakuwa Amekutengenezea” Ndugu Yangu Mungu Yupo, Ukatae Ukubali………………… Kuna ule mtazamo wa kuwaona watu ambao wamefanya mambo makubwa, na wale wenye ushawishi mkubwa sana kuwa hao ni watu wasio na makossa kabisa.… Read More »

511; Unakimbilia Wapi? Tazama Pembeni Yako.

 Haya Ndio Maisha yetu kwenye vitu vingi tunavyopitia kila siku, Soma kisa hiki ujifunze: “Habari kaka Jacob, ninaomba ushauri wako kuhusu hili. Ni mwaka wa tatu sasa tangu nikutane na binti mmoja na nikampenda sana. Nina tabia moja huwa sikati tamaa haswa pale ninapokuwa nimekipenda kitu Fulani maishani mwangu. Nimekuwa naamini kwamba ipo siku tu… Read More »

510; Ninajihisi Kama Mtu Aliekwama Kwenye Tope.

“Kaka Jacob naomba ushauri wako, sijui hata nifanyeje, huu ni mwaka wa 5 sasa nimekuwa najaribu kuingia kwenye mahusiano tofauti tofauti lakini naambulia kuachwa na kuumizwa. Mara ya mwisho nilikutana na mkaka mmoja ambaye tulianza nae mahusiano kwa haraka na motomoto sana lakini mwisho wake nikaja kuona anaanza kupunguza mapenzi taratibu, kaanza kupunguza mawasiliano na… Read More »

506; Nilimwona Akiingia Gesti Jana Jioni

Ni mara ngapi umewahi kuambiwa kuhusu wengine, mfano; “Nilimwona Fulani akiingia Gesti Jana”, “Fulani ana Mwanamke Mpya” na mengine mengi. Ukweli ni kwamba huenda umeyasikia sana kutoka kwa watu au hata wewe ulishawahi kumwambia mtu. Sasa nikwambie kitu kimoja, hayo ni maoni tu ya watu ambayo hayana ukweli halisia. Ngoja nikupe kisa hiki, Miaka michache… Read More »

504; Nyama Kilo 1 ni Tsh elfu moja.

Embu jiulize leo bei ya nyama kilo moja ni Tsh elfu tano hadi elfu saba kulingana na maeneo, sasa ukipita mahali ukakuta kuna nyama ya ng’ombe safi kabisa imenona wanauza kilo moja shilingi elfu moja utavutiwa kwenda kununua? Jibu rahisi sana na ambalo kila mmoja atafanya ni HAPANA. Na itakuwa hapana kwasababu haiwezekani nyama iuzwe… Read More »

493; USIWATHIBITISHIE. (DON’T PROVE THEM WRONG)

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiona watu wanafanya vitu mbalimbali kama ujasirimali, biashara fulani, kazi Fulani, ili tu kuwathibitishia watu fulani waliokuwa wanawaona wao hawafai. Mfano mtu aliambiwa wewe hujawahi kuweza kitu hutaweza biashara. Anaingia kwenye biashara kwa hasira ili tu amthibitishie yule mtu kwamba anaweza. Unaweza kuambiwa wewe huwezi kupata kazi Fulani kwasababu huna elimu… Read More »

487; KUNA WATU UMEWAZIDI VITU VINGI, LAKINI WANAFANIKIWA, ZIJUE SABABU ZINAZOKUKWAMISHA.

Umeshawahi kusikia mtu anasema, “Mbona kama wamempendelea yule! sionagi cha maana anachokifanya wala simuelewagi!!” Mwingine anadiriki kusema, “Atakuwa ametoa rushwa kuipata ile nafasi”, “Atakuwa anajuana na mtu kule ndio maana amependelewa” Je na wewe unafikra za aina hii? Ukiona wenzako wanafanya vizuri unafikiri wamependelewa au wana bahati Fulani? Haujawahi kuamini kwamba watu hawa wamefanikiwa kwa… Read More »

484; Ukiachwa Ni Nani Anakuwa Amepoteza?

Nilimpenda sana, nilimwonesha mapenzi yote, nilimpa kila alichokuwa anataka lakini nimeambulia kuachwa. Hayo ni mojawapo ya maneno ambayo watu wengi wamekuwa wakiyatoa baada ya kuchwa na wale waliokuwa wanawapenda sana. Nimetafakari nikajakugundua kama ni kweli ulikuwa unamfanyia mambo yote mazuri na kumpa kila alichokuwa anataka halafu akaja akakubwaga ukweli ni kwamba sio wewe uliepoteza bali… Read More »