KITABU: NUKUU ZA MAISHA.

Nukuu za Maisha (Malengo, Mafanikio, Mahusiano n.k) ni Kitabu kinachokupa muongozo wa maneno ya kutafakari kila siku asubuhi ili uweze kuwa na siku bora na yenye mafanikio. Kitabu hiki kina nukuu 400+ ambazo zinakupa uwezo wa kufikiri vizuri, kuishi kwa furaha na kuweza kusonga mbele katika kile unachokifanya. Nukuu za Maisha ni mjumuisho wa nukuu […]

KITABU: Mafanikio Kwenye Biashara.

Kitabu hiki kimebeba uhalisia wa Maisha ambayo nimeishi na kujifunza kutoka kwa wengine. Pamoja na kitabu hiki kubeba mambo mengi mazuri sana, bado inakupasa wewe uwe mchukuaji wa Hatua kwa kila unalojifunza ndani ya kitabu hiki. Usiishie kusoma na kuburudika kama msomaji wa hadithi bali uweze kuchukua Hatua hata kama ni ndogo lakini inayoleta mabadiliko kwenye […]

KITABU: Usiishie Njiani, Timiza Ndoto Yako.

Kitabu hiki ni maalumu kwako wewe ambaye unataka ndoto yako itimie. Kitabu hiki ni kwa ajili yako wewe ambaye bado hujapata mwelekeo wa Maisha yako. Utapata mwongozo kwa ajili ya kujitambua. Unapata Nini kwenye Kitabu? Utafahamu Umuhimu wa Maono kwenye Maisha yako. Utafahamu maswali 8 ambayo unapaswa kujiuliza na majibu yake ili uweze kusonga mbele. […]

KITABU; Mbinu 101 za Mafanikio. – Jacob Mushi

Kitabu hiki ni mkusanyiko wa makala ninazoandika kila siku za HATUA ZA MAFANIKIO. Nimechambua makala 101 ambazo ukizisoma zinaweza kukupa mbinu na maarifa ya kukuwezesha usonge mbele zaidi kwenye kile unachokifanya. Kitabu hiki cha Mbinu za 101 za Mafanikio Kimejumuisha , Mbinu za Maisha na mafanikio, sms za mafanikio, siri ya mafanikio katika biashara, nguzo za mafanikio katika Maisha, siri ya mafanikio […]

KITABU; Siri 7 za Kuwa Hai Leo

Kitabu hiki nimeandika kwa ajili yako. Kuna mambo mengi sana ya kujifunza ndani ya kitabu hiki na nina imani kitakua ni sababu ya wewe kusogea katika eneo lile ulilokua na kwenda mbele Zaidi. Utajifunza, Jinsi ya Kujua Kusudi Lako, Siri na Sababu za Kuwepo Hapa Duniani, Kugusa maisha ya wengine, Kufikia Ukuu, Kufika kilele cha Mafanikio, […]

KITABU: Mwongozo wa KILIMO CHA TIKITI MAJI

Baadhi ya Yaliyomo kwenye Kitabu hiki: Utajifunza shughuli zote za shambani kuanzia kuandaa shamba, upandaji, umwagiliaji, uwekaji mbolea, palizi, uvunaji n.k Vigezo vya kuzingatia katika uchaguaji wa shamba zuri pamoja na mbegu nzuri Utawafahamu Wadudu waharibufu na namna ya kuwadhibiti kikamilifu, pia Magonjwa yanayoathiri sana tikiti maji na namna ya kuyathibiti Utajifunza uchavushaji (pollination) kwenye […]