Katika maisha haya kamwe usimlaumu mtu yeyote kwasababu ya kushindwa kwako au kufeli kwako jambo fulani, kwasababu kulaumu hakuibadilishi hali bali kunatengeneza tatizo lingine linaitwa KiNYoNgO.

Hakuna mtu aliyetuma barua ya maombi kwa MUNGU azaliwe katika familia fulani yenye hali fulani au uzuri fulani, Wote tumezaliwa tumejikuta watoto wa fulani na fulani, Wengine wamezaliwa wamejikuta kwenye ndani ya kasri wamezungukwa na wahudumu kila pande.

Wengine wamezaliwa wamejikuta kwenye banda linalovuja kiangazi na kuchoma jua masika,
Wengine wamezaliwa kwenye elimu yaani baba professor mama Daktari.

Wengine wamezaliwa tu wamekuta mama anapigwa vibao anaburuzwa,
Mwingine amezaliwa amekuta mama yake anajiuza mwili,mwingine amezaliwa mahali watu wanatumia madawa ya kulevya,
mwingine amezaliwa mahali watu hawajawahi enda shule wala kufanikiwa
Wengine wamezaliwa tu wazazi wao wakafariki papo.

Mwingine amezaliwa amezungukwa na chupa za bia, mwingine vichochoroni, mwingine kanisani,mwingine vitani kwenye mabomu na risasi….
Kila mtu na alivyozaliwa ndio maisha..

Tatizo sio kuzaliwa hapo, kwenye taabu na shida nyingi Tatizo ni kuendelea kuwa hapo….
Kila mmoja Mungu amemwandikia story yake ya Ushindi ni Wewe Kuamua kuchukua hatua na kutoka kujikwamua kwenye shida hiyo…..

Mradi upo hai unaweza kuvuka……..
MSHUKURU MUNGU KWA ZAWADI HII YA MAISHA na kuyatumikia kwa ajili ya UTUKUFU WA UFALME WAKE ALIYEKUWEKA

*kuzaliwa zizini haimaanishi uishi hadi ufie zizini*
Waweza zaliwa zizini ukaishi Ikulu na kuishia Ufalmeni

By
Theofrida Gervas

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading