“If you don’t quit, and don’t cheat, and don’t run home when trouble arrives, you

can only win.” – Shelley Long

Zinapofika nyakati za matatizo kama uispoacha, usipofanya udanganyifu na wala usipokimbia kurudi kule ulipopazoea ni lazima ushinde. – Shelley Long

Hakuna hata sehemu moja umeona mtu ameacha kupambana au kufanya kile anachokifanya kwasababu kinamletea matokeo mazuri. Kila mmoja wetu atapenda kuendelea kufanya Zaidi na Zaidi kwasababu kuna matokeo mazuri. Lakini ili uweze kuwa mshindi kweli kweli ni lazima uonyeshe uimara na utayari wako wa kuendelea nyakati za matatizo na ugumu.

Kila mmoja atafurahia sana anachokifanya wakati mambo yanakwenda vizuri. Kila mmoja atajisiikia vizuri sana pale ambapo jioni akihesabu fedha anaondoka na faida kubwa. Lakini zile nyakati za huzuni ndizo zinaonyesha ukweli kama wewe ni mshindi.

Lazima ujue kuwa huwezi kufurahi nyakati zote. Kuna vipindi utapitia vitakuhitaji uwe mgumu usiekubali kushindwa.

Ndoto yako yako itakwenda kutimia tu pale ambapo utaamua kutokurudi nyuma bila ya kujali ni hali gani inaendelea. Kuna nyakati utajihisi upo peke yako lazima pia ukubali kuendelea kupambana bila ya kukata tamaa.

Wapo watu watakaokuja na kukwambia achana na hicho unachokifanya kwasababu wameona hakina maslahi. Kwako wewe unapaswa kujua ni kitu gani uliona wakati unaanza? Ile picha picha usikubali ififie moyoni mwako. Endelea kuitazama kila wakati unapokuwa kwenye hali ya kukata tamaa.

Nyakati pekee watu wanakata tamaa na kurudi nyuma ni nyakati ngumu. Na hizi ndio nyakati za kuchambua washindi wa kweli.

Ni mimi Rafiki Yako,

Jacob Mushi

USIISHIE NJIANI

Piga Hatua, Timiza Ndoto Yako.

 

Jipatie Vitabu vya Biashara na Mafanikio Hapa.. BONYEZA MAANDISHI HAYA

Tengeneza Kipato kwa kupitia Blog Bonyeza hapa.. BONYEZA MAANDISHI HAYA

Karibu Kwenye Kundi Maalumu la WhatsApp https://jacobmushi.com/whatsapp/

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading