Inawezekana kuna mtu unamngoja aje afanye jambo kwenye Maisha yako ili yabadilike. Inawezekana kwenye akili yako unasubiri ipo siku mambo yatakaa sawa na kuwa marahisi Zaidi ya sasa. Inawezekana pia kuna muujiza Fulani unautegemea kwenye akili yako utokee ndio kila kitu kibadilike kwenye Maisha yako.

Napenda kukwambia Rafiki huyo unaemngoja afanye yote hayo anakusubiri wewe uchukue Hatua ndio aonyeshe ushirikiano na wewe. Ukweli ni kwamba hakuna mahali umeambiwa hali itakuja kuwa nzuri hata kama umeahidiwa hivyo hali haitakuwa nzuri kwako kwa kuisubiri. Hakli itakuwa nzuri kwa wale ambao wanachukua Hatua kila siku kwenye Maisha yao.

Kipindi pekee ambacho muujiza ulikuwa unamfata mtu ni kile cha Yesu pekee. Huku kwetu sasa hivi unapaswa kufanya vitu na ukutane na muujiza wako Njiani. Lazima uamue kabisa kwamba nakwenda kuchukua Hatua hii na hadi nione ile Ndoto yangu imeanza kuwa kweli.

Usijidanganye hata siku moja kwamba hali itakuja kubadilika, hakuna hali inayobadilika bila ya kubadilishwa ndugu yangu. Lazima ukubali kuhusika katika mchakato wa mabadiliko kwenye Maisha yako. Ukiendelea kubaki hapo unasubiri muujiza na mabadiliko ambayo hujayafanyia kazi ni sawa na anaesubiria kwenda kuvuna kwenye shamba ambalo hajapanda.

Unajua ombaomba wa barabarani hata ikitokea siku amepewa pesa nyingi sana za kutosha kwenye kufanya aondoke kwenye uomba omba bado atarudi tena kesho akitegemea atakuja mwingine ampe nyingi tena Zaidi. Usikubali akili yako iwe kama ya mtu wa aina hii. Unapaswa kujua namna ya kutengeneza Maisha yako mwenyewe bila kutegemea mabadiliko ambayo yanakuja yenyewe.

Labda nikwambie kwamba mimi nilipokuwa mdogo tulikuwa na tabia ya kwenda kupita kwenye mashamba ya watu na kukusanya mabaki ya mahindi baada ya kuvunwa. Ukweli wa Maisha ya wengi yako hivi. Hata mwaka ukiwa wa mavuno mengi bado hawafaidi chochote kwasababu wao wanasubiria masazo ya wale waliovuna. Sasa usitegemee waliovuna wakubakishie masazo mengi kwasababu tu walivuna mahindi mengi.

Lazima ukubali kuwa mtu anaechukua Hatua na kutetea Maisha yake. Toka hapo ulipo Rafiki yangu. Usikubali kubaki sehemu moja muda mrefu, hakikisha unakuwa bora kila wakati. Hakikisha unaongezekana viwango.

Ni mimi Rafiki Yako, Jacob Mushi

#UsiishieNjiani

“Piga Hatua, Timiza Ndoto Yako.”

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading