Wakati wa Asubuhi Ndio wakati ambapo watu wengi wenye mafanikio huanza siku zao. Wengi wanaamka mapema ila sio kwasababu ndoto zao zinawasukuma, wengine wanawahi kuamka kwasababu bosi wake ni mkali akichelewa.

Asubuhi akili inakuwa haijachoka hivyo chochote utakachokifanya asubuhi kinakuwa na matokeo bora sana.

Asubuhi hakuna usumbufu, watu wengi wanakuwa wamelala, mifugo, redio zimezimwa, Watoto hawasumbui hivyo unakuwa na utulivu wa kufanya mambo yako vizuri.

Asubuhi ndio muda ambao mwili wako pia unakuwa umechangamka.

Ukiamka mapema unaanza kujiengenezea ushindi mdogo mdogo hivyo siku yako yote inakwenda kuwa ya kishindi na yenye matokeo chanya.

Ukiamka asubuhi na mapema ukaipangilia siku yako unajitengenezea matokeo chanya.

Kama utaamka asubuhi na mapema na ukaanza kujikumbusha yale malengo yako makubwa utakuwa na hamasa kubwa sana ya kufanya kazi siku hiyo na utapata matokeo mazuri Zaidi.

Ukiamka asubuhi ukasoma kitabu unaweza kukielewa vizuri Zaidi kuliko wakati wa mchana kwasababu unakuwa na focus Zaidi.

Nawashauri wote wale mliokuwa hamuwezi kuamka asubuhi na mapema muanze kuamka mapema. Wale mliokuwa mnaamka mapema lakini mnafanya mambo ya kawaida kabisa basi muanze kuyafanya haya niliyoelekeza kwenye Kanuni yetu.

Mafanikio yako yaanza asubuhi, ushindi unaanza asubuhi, kila kitu ni asubuhi na mapema. Usiamke ukaanza kutembelea kwenye mitandao ya kijamii badala yake amka uanze kufanya yale ya muhimu kwako.

Mwanzo utakuwa mgumu lakini endelea kuwa mvumilivu na kurudia rudia hadi ikae kwenye utaratibu wako wa kila siku.

 

Ubarikiwe sana,

Rafiki Yako, Jacob Mushi

www.jacobmushi.com/huduma

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading