Siko zote akili ya mwanadamu inaposhindwa kujishughulisha hivyo hutafuta sababu rahisi ambayo itamfanya aendelee kubaki vile alivyo. Hatari kubwa inakuja hapo ni kwamba hauwezi tena kubadilika kwasababu kitendo cha kusema matajri ni wachawi na washirikina maana yake huwezi kuwa tajiri wewe. Kwasababu ukisema uwe tajiri umeachagua kuwa mshirikina na mchawi. Kitu cha ajabu ni kwamba ukimwambia mtu huyu anaesema matajiri ni wachawi atoe uthibitisho hana cha maana cha kukuambia. Zaidi ataanza kukueleza hadithi alizozisikia kwa watu.
Ndugu yangu hauwezi kufanikiwa nje ya kile unachokiamini hata siku moja. Kama unaamini Kufanikiwa ni kufanya kazi kwa bidii basi bidii ndio itakuletea mafanikio. Badilisha Imani zako ulizonazo na maisha yako yatakwenda kubadilika. Hakuna kazi ngumu kama kubadilisha imani ya mtu.
Leave a Reply