Leo nakumbuka siku yangu ya kuzaliwa, nimetimiza miaka kadhaa hapa duniani. Katika kutafakari mambo mbalimbali na kujiuliza maswali nilijikuta katika mawazo haya, “Mimi sijawahi kumuomba Mungu aniumbe binadamu, sasa inakuaje nikikosea ameahidi adhabu mbalimbali?” kwanini niadhibiwe kwa Maisha ambayo hata sijayachagua kuishi?

Ukweli ukitafakari hayo maneno yako kama yana ukweli Fulani ndani yake. Lakini hupaswi kuishia hapo katika tafakari yako unapaswa uendelee kuchimba ndani Zaidi.

Mimi pia sikuishia hapo, katika kutafakari nikajikuta nawaza tena, hivi ni aina gani ya mifugo huwa inatuomba tuiofuge? Paka alishawahi kuomba afugwe na binadamu? Je mbwa? Kuku? Mbuzi bata? Nikaja kugundua kumbe hii mifugo pia haijawahi kuomba kufugwa nasi, ni sisi wenyewe tuliafanya maamuzi ya kuwafuga kutokana na uhitaji wetu.

Hivyo basi endapo paka ataharibu kitu huwa tunamuadhibu, mbwa akimuuma mtoto lazima apigwe kipigo cha uhakika, vivyo hivo Wanyama wengine. Sasa tujiulize yeye Mungu sio zadi ya sisi binadamu? Kama tunaweza kuwaadhibu Wanyama hata kufikia kuwaua kwasababu ya makossa mbalimbali na Wanyama hao hawajawahi kuja kutuomba tuishi nao iweje kwa Mungu tushangae?

Hapo ndipo nikapata majibu ya kwamba lazima tukubali kuishi vile Mungu anataka tuishi na tukikaidi basi tusimlaumu kwa lolote baya litakalokuja juu yetu. Kama ambavyo Wanyama hupata adhabu mbalimbali hata kwa majirani ndivyo kwa upande Fulani Maisha yetu yako hivyo.

Tuendelee kumpenda Mungu, kutenda yaliyo mema, kuwapenda wanadamu wenzetu na kuishi vizuri. Ni kweli hukuomba kuumbwa lakini hupaswi kuishi utakavyo kwasababu upo kwenye dunia yenye mwenyewe. Yeye alieiumba dunia anataka uishi hapa duniani vile anavyotaka yeye na sio vile unavyojiamulia wewe.

Nakutakia kila la Kheri katika Kutimiza mapenzi ya Mungu Wako.

Rafiki Yako Jacob Mushi.

www.jacobmushi.com

12 Responses

  1. Asante kwa ujumbe murua kwa hakika wengi huwa hatutafakari kwa kina ndiyo maana huwa tunaishia kulalamika kuwa Mungu hayuko Fair, ubarikiwe sana kaka Jacob

  2. mwanzo nlisoma kichwa cha habari tuu nikaona sikubaliani nawe nkaachana nayo, lakini nlipopata neema ya kuisoma yote nimekuelewaMungu atupngoze tutende mema

  3. Ubarikiwe Kwa ujumbe mzur mtu wa Mungu ! Nilikuwa najiuliza Ni nn hasa hiki anataka kutuletea huyu ndgu! Wakat mwingine hawa wanyama tumewaadhibu bila Hata ya sababu . Lakin point ya mwish Na kubwa Ni kwamba tunapaswa kuishi si Kama tutakavyo Ila Kama atakavyo Mungu wetu aliyetuumba

  4. Asante Sana brother.. Mara zote nafuatilia hata pale nnapokosa kushukuru kwa kuandika basi huwa nnakushukuru hata huku nikiwa mwenyewe kimoyomoyo.. Mungu azidi kukubariki..

  5. Mungu akubariki sana na azidi kukuza kipawa chako na kukuongeza hekima zaidi na zaidi na akujalie kuwa na maisha marefu yenye heri na kujaa Neema yake. Usiishie njiani.

Leave a Reply to TumainiCancel reply

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading