Mtazamo ni vile ambavyo mtu amejengewa au amejijengea maana fulani au imani fulani juu ya jambo fulani. Mtazamo waweza kutengenezwa kutokana na mazingira unayoishi vitu unavyosoma, kutazama na kufuatilia. Mtazamo pia unaweza kutengenezwa na aina ya watu unaojihusisha nao kila siku.

Mfano unakaa na watu ambao wanasema hawawezi kuuza bidhaa kwa kumfata mtu na kunwelezea faida za bidhaa. Lazima utajikuta na wewe unaanza kuiga na kubadilisha mtazamo wako hasa kama ulikuwa huamini hivyo.

Unakaa na watu ambao wanapenda kulalamika na kuona ugumu kwenye kila jambo lazima utajikuta unaanza kufanana nao kimtazamo.

Mtazamo wako juu ya mambo unayopitia ndio unaamua wewe uwe kwenye hali gani.
Unaweza kukuta watu wawili wanapitia hali ngumu zinazofanana halafu mmoja ana furaha kama kawaida huku mwingine akilalamika kila wakati.

Watu wengi wanalalamika hawana mtaji wa kuanzia biashara lakini si kweli hawana. Mtaji wanao ila walishajiambia kwamba kazi fulani siwezi kuifanya kabisa.
Siwezi kuuza kwa namna hii.

Badili mtazamo wako ili uweze kuona uwezekano kwenye kila hali unayopitia.
Mtazamo wako ndio unashape maisha yako.

Ni mimi Rafiki Yako,
JacoMushi.

USIISHIE NJIANI

Piga Hatua Timiza Ndoto Yako

Pata vitabu vya biashara na mafanikio hapa www.jacobmushi.com/patavitabu

Jipatie Blog na Utengeneze Kipato www.jacobmushi.com/jipatieblog

Jiunge na Kundi Maalum la WhatsApp www.jacobmushi.com/whatsapp

2 Responses

Leave a Reply to AbduliwaqirCancel reply

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading