Unaweza kuwa na kila kitu ambacho wengine kwa nje wanaona ni kizuri lakini kumbe yote hayo ni matokeo ya mawazo ya watu wengine juu yako.

Kama unachokifanya hakijatoka ndani yako utaishi Maisha yako yatakuwa ni kifungo cha mawazo ya wengine .

Kutokana na maoni ya watu wengine juu ya Maisha yanavyotakiwa kuwa umejikuta upo ndani ya maoni yao na mawazo yao bila kujua. Uliambiwa kwenu lazima mtoto wa kwanza awe daktari na wewe ukaenda kusomea udaktari sio kwasababu imetoka ndani yako bali kwasababu ni mawazo ya watu wengine.

 

Tuna watu wengi wanakuwa waovu na wabaya kwenye kazi wanazozifanya kwasababu tu sio kitu walichozaliwa kuja kufanya. Kuna kazi ambazo wengi walikimbilia kufanya kwasababu tu Maisha yalishakuwa magumu kwao na wakakosa pa kwenda.

Unaweza kuwa na mshahara mzuri na kila kitu kizuri lakini kamwe huwezi kuwa na furaha hadi ujue ni kwanini upo hapa duniani.

 

Ukiona mtu anafanya mambo ya ajabu kwenye kazi yake lazima kunakuwa na matatizo. Hii ni kwasababu wengi wanafanya vitu ambavyo walilazimishiwa. Wengi wanafanya kazi kwasababu walikuta watu wanafanya kazi duniani.

Wengi wanaishi Maisha wanayoishi sio kwasababu ni sahihi bali ni kwasababu wamekuta binadamu wengine wanaishi. Hata kama kulikuwa na makossa yaliyokuwa yanaendelea toka zamani wanakuwa wanayaendeleza.

Jiulize maswali magumu juu ya kile unachokifanya je ni kweli umezaliwa uje kufanya? Ni bora ufanye jambo ukiwa unajua baada ya muda Fulani utaachana nalo na kuendelea na mambo mengine kuliko kuwa mtu asielewa kwanini anafanya. Wengi wanafanya kwa kufuata mkumbo na sio kwasababu wanachokifanya ni sahihi.

 

Lazima ukubali kujua Maisha unayoishi umefuata kama ulivyokuta wanaishi au ni namna ambavyo Mungu ametaka uje kuishi hapa duniani.

 

Ni mimi Rafiki Yako,

Jacob Mushi

USIISHIE NJIANI

Piga Hatua, Timiza Ndoto Yako.

Jipatie Vitabu vya Biashara na Mafanikio Hapa.. BONYEZA MAANDISHI HAYA

Tengeneza Kipato kwa kupitia Blog Bonyeza hapa.. BONYEZA MAANDISHI HAYA

Karibu Kwenye Kundi Maalumu la WhatsApp https://jacobmushi.com/whatsapp/

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading