Habari Rafiki, Leo ni siku nyingine tena ambayo tumepewa kama zawadi kwa ajili ya kwenda kuyafanya Maisha yetu yawe bora Zaidi.

Jisemeshe Maneno Haya Kabla Hujatoka Kwenda kufanya Chochote.

“NACHUKUA HATUA, NAJIFUNZA, NAWEKA JUHUDI NA BIDII, NAVUMILIA.
MAFANIKIO NI HAKI YANGU, EEH MUNGU NIWEZESHE.”

Watu wengi hutafuta njia rahisi za kufanya mambo yao, sasa tatizo halipo kwenye njia rahisi. Swali la kujiuliza ni je hiyo njia inaleta suluhisho la kudumu kwenye tatizo!?

Mara nyingi njia rahisi zinaweza kuwa sababu ya mambo kufanyika chini ya kiwango. N wengi huzitafufa njia hizi ili kukwepa gharama fulani.

Sasa zile gharama ambazo zinakwepwa huja kuleta gharama kubwa zaidi mbeleni.

Kwenye safari ya mafanikio usipende sana kuangalia kirahisi ni kipi bali angalia sahihi ni kipi. Je kinaleta yale matokeo yanayotakiwa?

Penda kujiuliza maswali ili ujue matokeo ya hatua unazotaka kuchukua.

Usikubali kukwepa kulipa gharama maana utakuja kuilipa tu siku moja.

Ni mimi Rafiki Yako, Jacob Mushi
#UsiishieNjiani
“Piga Hatua, Timiza Ndoto Yako.”
https://jacobmushi.com/patavitabu/

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading