Habari Rafiki, Leo ni siku nyingine tena ambayo tumepewa kama zawadi kwa ajili ya kwenda kuyafanya Maisha yetu yawe bora Zaidi.

Jisemeshe Maneno Haya Kabla Hujatoka Kwenda kufanya Chochote.

“NACHUKUA HATUA, NAJIFUNZA, NAWEKA JUHUDI NA BIDII, NAVUMILIA.
MAFANIKIO NI HAKI YANGU, EEH MUNGU NIWEZESHE.”

Mojawapo ya watu ambao wanaishi kwa mateso duniani na huzuni ya ndani kwa ndani ni wale ambao wanafanya vitu ili kuwaridhisha wengine.

Unavaa mtindo fulani ili umvumtie mtu fulani akupende, ndugu yangu kama hujaajiriwa na shirika la kijasusi basi unajitesa bure.

Unabadili kabisa mtindo wa maisha yako ili tu umvumtie mtu fulani au uendane na aina ya watu fulani.

Ukijikuta unaacha kuwa wewe na kuanza kubadilika kuwa mtu mwingine ujue unajipoteza. Ipo siku utakuja kuona ulikuwa unapoteza muda bure.
Hao unaotaka kuwavutia siku wakigundua sura yako halisi watakukimbia.

Unachopaswa kufanya ni kuhakikisha unakuwa wewe na unajiongeza uwe bora kila siku. Watu sahihi wataambatana na wewe.
Waache watu wakupende vile ulivyo maana hutapata shida kufanya vitu vya ziada ili upendwe.

Ishi maisha yako vile ambavyo unapata furaha hata ukiwa mwenyewe watu sahihi watakuja kwako.

Ni mimi Rafiki Yako, Jacob Mushi
#UsiishieNjiani
“Piga Hatua, Timiza Ndoto Yako.”
https://jacobmushi.com/patavitabu/

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading