Unajua hakuna kisichowezekana kwenye dunia hii endapo utakuwa umeweka nia ya dhati ya kutaka kufanikisha. Endapo utaamua kwamba hakuna chochote kinachoweza kukuzuia tena, ukikubali kila kitakachokuja mbele yako kiwe kibaya au kizuri utaamua kukitumia kama silaha ya kukusogeza mbele.

Nikuambie kitu mimi sijazaliwa kwenye familia yenye nafuu ya aina yeyote, nimewahi kukosa ada ya shule, nimewahi kukosa nguo za kuvaa, nimewahi kulala njaa pia. Unaweza kusoma Zaidi hapa www.jacobmushi.com/kuhusu. Kuna nyakati niliwahi kukosa ada ya shule nikasema niende nikaombe msaada mahali. Nikaambiwa hatuwezi kukusaidia mwambie mama yako akusomeshe.

Hapo ndipo nilipata hasira sana nikasema sitasoma lakini nitafanikiwa, sitaenda chuo kikuu lakini lazima siku moja historia ya Maisha yangu isomwe na walioenda chuo kikuu. Na ukweli hili linakwenda kutokea, sio kwa bahati mbaya, bali ni kwasababu nilishafanya maamuzi haya miaka mingi iliyopita. Ndugu yangu wewe unakutana na changamoto unarudi nyumbani unalia unasema basi bado hujajua uchungu wa Maisha.

Changamoto yeyote inayokuja mbele yako unapaswa kusema nitaitumia kusogea mbele, sitakubali inifanye nirudi nyuma. UGUMU WA MAISHA NA MAZINGIRA YAKIKUIKANDAMIZA CHINI USIONEKANE NA WALA USISIKIKE, JITAHIDI KUTAZAMA KILA FURSA INAYOKUJA MBELE YAKO ILI UWEZE KUINUKA HATA KAMA ILIKUWA NI KUPIGA KELELE TU PIGA KWA NGUVU ZOTE. ENDELEA KUFANYA HIVI KILA WAKATI.”

Chochote kinachokuja mbele yako hata kama ni kifo kinataka kutokea usikubali kuruhusu iwe ni mwisho wako mbaya fanya kila uwezalo umalize kwa ushindi. Kamwe usiongee maneno juu yako yale usiyoyataka. Acha watu waseme maneno mabaya kwako, acha waseme huwezi, acha waseme wewe kwenu hamtakaa mfanikiwe, acha waseme wewe hujawahi kufanikisha chochote cha maana lakini kamwe wewe usijisemee maneno kama hayo. Jisemee maneno ya ushindi. Hata kama jana huweza kufanya chochote leo unaweza kufanya.

Usikubali chochote kikuzuie, unajua ukiwa umefungiwa kwenye chumba chenye giza halafu hakuna sehemu ya kutoka wakati mwingine unaweza kuwaza kukata tamaa. Lakini bado kunakuwaga na nafasi kila wakati ya wewe kutoka, na nafasi hiyo ni ile siku mpya unayoendelea kuiona kila siku. Kama umeona jua tena leo maana yake ipo nafasi ya wewe kutoka kwenye hicho chumba chenye giza.

Bado naendelea kusema, kama bado hujafa mpaka sasa, basi usikate tamaa kwenye ndoto yako.

Nakutakia Kila la Kheri

Rafiki Yako Jacob Mushi.

www.jacobmushi.com/coach

2 Responses

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading