Siku zote kama unaishi na watu ambao unaona kama wamekuzidi vitu vingi, utakuwa unajiona wewe ndio hujakamilika. Unaweza kuona wengine wanavaa vizuri kuliko wewe, wanakula vizuri kuliko wewe, wanaendesha magari mazuri kuliko wewe, wana wenza wazuri kuliko wewe. Hii inasababishwa na wewe kujisahau kabisa na kutoangalia vile vizuri ambavyo umebarikiwa.

Kama utatumia muda mwingi kutazama vile ambavyo huna utaviona vingi sana. Ukiwaangalia wengine unaweza kusema wana furaha kwenye ndoa yako kuliko ndoa yako. Lakini ukweli upo hivi, hii inatokea kwa watu wengi, inawezekana yule unaedhani ana furaha kuliko wewe hata yeye ana vitu ambavyo havifurahii na akiviona kwako anakuona wewe umemzidi.

Hivyo basi badala ya kukaa na kuwatazama wengine jitazame wewe umebarikiwa vitu gani. Mshukuru Mungu kwa hivyo na uvifurahie sana, kwasababu kuna siku vinaweza visiwepo tena. Kuna msemo unasema “Unalalamika Huna Viatu Kuna Wengine Hawana Miguu” yaani kwasababu huna viatu usijione wewe huna kila kitu mshukuru Mungu amekupa Miguu ambayo unaweza kuitumia kwenda kutafutia viatu kwasababu kuna watu ambao hawana hiyo Miguu yako.

Kuna vitu vingi sana umebarikiwa ana wengine hawana, jikubali, jione umebarikiwa na baraka za Mungu zitadumu kwenye Maisha yako. Kamwe usitumie Maisha ya wengine kama kipimo cha kupimia Maisha yako. Yale malengo makubwa uliyoyaweka ndio yawe kipimo chako. Jitazame miaka kumi ijayo kisha ujione bado una safari ndefu ya kufika huko.

Ukiweza kujikubali utaanza kuona mengi yanakuja kwenye Maisha yako, ukianza kumkubali huyo uliepewa au uliemchagua utaanza kuona vitu vingi vizuri Zaidi ndani yake. Anza kwa kushukuru kwa kile ulichonacho ili upate Zaidi.

Ubarikiwe sana,

Rafiki Yako, Kocha Jacob Mushi

6 Responses

  1. asante sana mwalimu wangu mzuri Jacob Mushi kiukweli ninapitia mengi nashukuru kila nikisoma post zako zinafanya kazi ya kunisimamisha kila dakika,
    kaka nimepitia magumu sana mwezi wa kumi na mbili natamani uishi nianze upya hapa nilipo sina hata simu yakuweza kusoma post zako huko fb wala inst kutokana na watu kuniibia simu zangu pamoja na kiasi cha pesa shilingi laki tano na baada ya kama siku nne kupita tena akaja kijana tunae mfahamu kumbe anafanya biashara amzao ni haramu kwakua hatukujua tulimkaibisha na baada ya hapo wakaja kumshika askari na hao askari walishindwa kumshika mtuhumiwa na baadae mume wangu akaingizwa katika matatizo ambayo yalihitaji pesa ya shilingi milion 10 kwani walisema watamfunga miaka 30 na kwakua yule kijana aliacha hadi kithibitisho katika gari yetu basi nilihangaika sana kuipata pesa mpaka nikafika hatua niseme niuze gari lakini siku ilofwata nikaomba mkopo katika ofisi nayofanyia na waliweza kunipa pesa kiasi cha shilingi milion tatu na moja nikaazima sehemu nyingine so nilipa hao askari kiasi cha shilingi milion nne kasoro laki mbili na wakamwachia mume wangu,
    nashukru tunauhai tutahangaika kusonga mbele ila mapito ya ulimwengu ni mengi ila kaka nakuhakikishia sijakata tamaa namwomba tu mungu anisaidie sana.
    ahsante sana

    1. Pole sana dada Agnes kwa changamoto hiyo kubwa sana. Kwanza naamini kwa kupitia hiyo changamoto yapo mengi sana umejifunza na yatakuwezesha uendelee kuwa bora zaidi.
      Usikate tamaa ya maisha anza upya, andaeni mpango wa kupunguza hayo madeni ambayo yametokea ili mrudi upya kuendelea na maisha. Kuna funzo Kubwa mmepata katika mapito hayo. Kikubwa ni kumshukuru Mungu kwasababu mpo hai na mmeweza kuvuka majanga hayo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *