Jaribu Tena, ndio nasema jaribu tena bila kujalisha umeshajaribu mara ngapi. Jaribu tena ukiwa na uhakika kwamba kuna jipya ulilojifunza kichwani kwako.

Jaribu tena bila ya kuhofu labda utakosea tena. Kama tayari kuna somo umepata kwenye kushindwa kwako basi utakuwa na ujasiri wa kujaribu tena.

Watu wengi hukata tamaa kabla hawajakaa chini na kujitazama ni kipi kinachosababisha washindwe.

Wewe usikubali kuwa kama watu wengi, anza kwa kuangalia ndani yako. Jua ni kitu gani hukijui, kwasababu kama unashindwa mahali ni kwamba kuna kitu hujakijua vizuri.

Kwa kujaribu tena unajiongezea nafasi ya kukishika vizuri kile ambacho ulikuwa hukijui.

Kabala Hujakata tamaa, jaribu tena, jifunze tena, chukua hatua tena, omba msaada tena.

Usikubali tu kirahisi na kupotelea njiani.

USIISHIE NJIANI, JARIBU TENA.

Kupata huduma mbalimbali ninazotoa tembelea kwenye link hii www.jacobmushi.com/huduma

Nakutakia Kila la Kheri.

Rafiki Yako

Kocha Jacob Mushi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *