Kwenye chochote kile ambacho unakitegemea katika kukuletea pesa iwe ni biashara au ajira  ni vyema kujiuliza swali hili kwamba, kutokana na mabadiliko yanayokuja kila wakati hasa ya kiteknolojia je nitabaki salama kwa muda gani?

Kama ni biashara basi angalia jinsi unavyoiendesha biashara yako sasa hivi na namna ambavyo mambo yanabadilika je unabadilika au unaendelea kutumia mifumo ya zamani?

Je endapo likatokea badiliko lolote la kuondoa mfumo ninaoutumia nitabakia salama?

Unatakiwa ujue kwamba kila siku kuna binadamu wanawaza namna gani wanaweza kuyafanya maisha yawe marahisi kwa kurahisisha upatikanaji wa vitu na huduma mbalimbali. Mojawapo ya vitu vinavyoangaliwa ni biashara yako pia.

Ni vyema ukajitengenezea tabia au mfumo wa kutotegemea aina moja ya uendeshaji ili usije kuanguka kibiashara. Kwasababu mabadiliko yakija hayakuhurumia kama ulijiandaa au hukujiandaa. Kama utatokea mfumo rahisi wa wateja wako kupata huduma au bidhaa unayoiuza halafu wewe pekee ukawa ndio hauna huo mfumo ujue unaweza kuangushwa kibiashara.

Lazima uangali mbele uone ni mabadiliko gani yanakuja na yanawezaje kuathiri kile unachokifanya. Ukiweza kutazama mbele vizuri unaweza kuwa na maandalizi ili lolote linaweza kutokea likuletee athari chanya kwenye biashara yako.

Ni hatari sana kubaki kwenye mfumo wa zamani huku ukidharau mabadiliko madogo madogo yanayokuja. Ni sawa na wale ambao walibaki na farasi zao wakadharau waliokuwa wanatengeneza magari mwisho wa siku unabaki na farasi wako wengi na hakuna wa kumuuzia maana wote wanataka magari.

Tazama mbele ona mabadiliko, jiandae.

Jacob Mushi

USIISHIE NJIANI

“Piga Hatua”

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading