Umeshawahi kusikia mtu anasema, “Mbona kama wamempendelea yule! sionagi cha maana anachokifanya wala simuelewagi!!”

Mwingine anadiriki kusema, “Atakuwa ametoa rushwa kuipata ile nafasi”, “Atakuwa anajuana na mtu kule ndio maana amependelewa”

Je na wewe unafikra za aina hii? Ukiona wenzako wanafanya vizuri unafikiri wamependelewa au wana bahati Fulani? Haujawahi kuamini kwamba watu hawa wamefanikiwa kwa juhudi walizoweka wewe unaamini tu kuna upendeleo Fulani wamefanyiwa?

Ukweli ni kwamba hutakaa uweze kufikia ndoto zako kama wewe huamini katika uwezo wa wengine. Kama ukiona wanaopiga hatua Fulani unaanza kudhani wametumia njia za mkato basi hata wewe itakuwa ngumu kufanikiwa. Hii ni kwasababu na wewe utaenda kutafuta njia za mkato halafu utafeli.

Wale watu ambao unaona wanafanikiwa kuliko wewe na ukitazama walichokifanya wala hakionekani kama ni kikubwa sana kuliko uwezo wako ni watu ambao wanajiamini. Ni watu ambao hawakujali sana kuwa wakamilifu waliamua kuchukua hatua vilevile walivyo na kilekile walichokuwa wanakijua. Wewe kwasababu unataka ujue kila kitu, unataka uwe na mtaji wa kutosha wenzako walianza hivyo hivo, wenzako walisumbua watu mbalimbali mpaka wakapewa nafasi na wakaonekana.

Kinachokukwamisha ni hiki hapa:

FIKRA POTOFU

Kikubwa kinachokufanya wewe uendelee kubaki hivyo hivyo ulivyo ni fikra zako potofu juu ya mafanikio ya wengine. Huamini kama mtu Fulani aliefanikiwa alitumia njia sahihi. Ufahamu wako umejazwa na fikra potofu ambazo zinakufanya wewe usichukue hatua na kubaki hapo hapo siku zote.

Fikra zako zinakwambia hata upambane vipi huwezi kufanikiwa kwasababu wakina Fulani walitoaga rushwa ndio maana wakafanikiwa. Kina Fulani walienda kwa mganga ndio maana wakatoka. Kina Fulani ni freemason ndio maana wamepata umaarufu mkubwa. Hizi fikra ukiwa nazo huwezi kufanya chochote utaishia kukaa na ujuzi ulionao, akili ulizonazo, bila kufika mahali popote.

Anza kwanza kubadili fikra zako ziwe chanya, ukiona dada mzuri amepandishwa cheo hata kama hana uwezo mzuri kuliko wewe acha kufikiri kwamba ametoa rushwa. Kwasababu hata wewe kuna kitu unaweza kukifanya vizuri na ukapandishwa cheo. Hata kama ni kweli alitoa rushwa wewe haikuhusu sana endelea kufanya vitu sahihi kwa ubora wa hali ya juu.

Tengeneza fikra chanya kwenye mafanikio unayoyataka amini kwamba waliofanikiwa walifanya kazi kwa bidii hawakukata tamaa. Hawakuwa wavivu kama wewe, hawakuwa watoa sababu kama wewe walikuwa wachukua hatua, walisumbua watu wa namna mbalimbali hadi wakapata fursa za kufanikiwa.

KUTOKUJIAMINI

Huwezi kufika sehemu yeyote ile kama hujiamini. Kama unajiona wewe huwezi. Kikubwa kinachowafanya uone wale wamefanikiwa lakini hawana hata uwezo mkubwa ni kwamba walijiamini sana. Hawakuangalia hawawezi nini bali waliangalia kile wanachokiweza na wakakitumia kwa nguvu zote.

Wewe ukisema usubiri ujue kila kitu ndio uanze utachelewa sana. Anza na kilekile unachokijua na kukiweza vizuri cha muhimu ni kujiamini. Mbele ya safari ndio utaendelea kuboresha.

Unaweza kuwa mmoja wa watu ambao unajua vitu vingi sana lakini huna hata kimoja ulichokifanyia kazi kwasababu tu hujiamini. Unataka ukianza tu uwe umefanya vizuri kuliko wote. Rafiki yangu hapo utachelewa sana. Huwezi kuanza kwa kufanya vizuri kila kitu lazima ukosee, lazima uanguke kisha usimame tena kama mtoto mdogo anavyojifunza kutembea.

KUSUBIRI UWE UMEKAMILIKA.

Ndio usisubiri hadi uwe na mtaji wote, usisubiri mpaka uweze kila kitu. Ukisema mpaka niweze kabisa kuna wengine wanaanza wakiwa hawajui na wanajifunza kwenye makossa yao. Kuna msemo unasema furs ani kama maembe wewe ukisubiri yaive wengine wanakula na chumvi. Maana yake wewe unaposubiri ukamilike wapo watu waanza wakiwa hawana chochote. Wako watu wanaanza na elfu kumi wakati wewe unasubiria ijae laki moja.

Wenzako wanaazima wanaanza wewe unataka kila kitu uwe umekinunua. Usipoteze muda wako kusubiri uwe umekamilisha kila kitu. Hata facebook ilipoanza haikuwa kama ilivyo sasa kuna vitu vingi sana wameendelea kuboresha na hata unavyosoma hapa wanafikiria kuboresha vitu vingine. Anza hivyo hivyo ukikosea utajifunza Njiani.

Usisubiri uje kupoteza milioni kumi anza na laki ikipotea utaumia kidogo lakini utakuwa umejifunza. Ukianza na milioni kumi ikapotea utaanguka presha ndugu yangu.

KUCHAGUA KUWA MKOSOAJI WA VITU VYA WENGINE BADALA YA MLETA SULUHISHO.

Ndio inawezekana wewe umechagua kuwa mtu ambaye unakosoa kila kitu na huku hujafanya chochote cha maana kwako mwenyewe. Wewe umekaa unasema Fulani ametoa hongo ndio maana anaitwa sana kwenye Tv kuliko mimi kumbe kuna mahali tu hujajua wakati wewe umekaa unawaza hivyo yenye anajenga mahusiano mazuri na urafiki na watu mbalimbali ambao wanampa nafasi.

Wakati wewe unapoteza muda na watu ambao wanalalamika na kukosoa tu wenzako wamekaa na watu walifanikiwa Zaidi na wanawashika mkono. Mwisho wa siku unaishia kusema wametoa rushwa, wameenda kwa mganga, wamependelewa, wana mjomba wao Tajiri na kadhalika. Utaendelea kubaki hapo kama hutoamua kutoka kwenye mkosoaji na kuwa mleta suluhisho

Nakutakia Kila la Kheri.

Rafiki yako Jacob Mushi.

www.jacobmushi.com/coach

2 Responses

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading