Nilipokua sekondari tulitumia barabara mbaya sana kuelekea shuleni kitu kilichofanya safari iwe ya kuchosha sana na yenye kuchukua muda mrefu sana.
Kipindi hicho barabara nzuri ya lami ilikua ikitengenezwa, kila nilipokua nikisafiri kwenda na kurudi shule nilitumia muda huo kujifunza juu ya ujenzi wa barabara!

Ujenzi wa barabara unapoanza unaudhi sana kwani miti hukatwa , udongo huchimbuliwa na miamba huvunjwa, ni kazi isiyotamanisha kuiangalia inapoanza,

Na watu wengi hawapendi kusafiri barabara inapojengwa maana safari huwa ya kuudhi na kuchosha sana!
Ujenzi wa barabara ya lami ni mfano wa mtu anayepitia mchakato kuelekea mafanikio,
Mambo yanayomtokea mengi huwa ya kuudhi na lengo ni kumuimarisha na mengine huja ili kumkatisha tamaa,
Dharau,kejeli,njaa,magonjwa,kuumizwa,kutokukubaliwa na mengine mengi yanayoudhi!
Mara nyingi watu humuepuka na hukwepa kuwa naye karibu kwa kuhofia shida anazopitia!
Na marafiki wengi waliokosa utu humuumiza mtu aliye ktk mchakato kwa kutokujua kesho yake kutokana na anayopitia!
Mfano wa barabara ikishakamilika kila mtu hufurahia na hutamani kuitumia na kuielezea jinsi ilivyojengwa na ilivyo bora!

Na mtu akishafanikiwa kufikia aliyoandikiwa ndipo kila mtu hutamani kuwa naye na hutamani kila mtu ajue kuwa anajuana nae!

Ili uwe mtu bora lazima upitie hatua mbalimbali mfano wa barabara ijengwayo,
Lazima upitie MCHAKATO ndio uwe bora zaidi!
Watu wa kawaida hawapitiagi hatua za ukuaji za kimchakato!

NB. Usiogope mchakato, usiogope watu kukuacha ukiwa mchakatoni
Songa mbele!

Uwe mtumishi wa MUNGU,una huduma,una vipaji, una ujuzi flani, lazima upite kwenye mchakato ili uwe bora!

Watu wote bora tunaowasoma kyk Biblia walipitia michakato tena migumu mnoooo!
Tukiwatazama kina Yusuphu,Musa,Yohana,Petro,Ibrahimu ni mifano mikubwa!
Tumwangalie MUNGU na tusonge mbele

#Noturning back
By Theofrida Gervas

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *