Kuna mtu yupo hospitali anamlilia Mungu ampe uzima ulionao, halafu wewe ni mzima na unakata tamaa.

Jacob Mushi

Unapotaka kukata tamaa kumbuka kwamba kuna watu ambao wanalilia nguvu ulizonazo sasa hivi. Kuna mtu anaipigania pumzi ya mwisho ili angalau aendelee kuwa hai.

Nataka ujue kwamba uzima ulionao ni fursa kubwa sana kwasababu ni nafasi ya kujaribu tena. Ni nafasi ya kujifunza kwenye makosa uliyofanya.

Kuna watu wamefanya mambo wakakosea na kukosea kwao kukawa sababu ya kupoteza maisha. Wewe ulie mzima unakubalije kusema huwezi kufanya tena.

Kila siku mpya unayoiona ni nafasi nyingine tena ya kuchukua hatua mpya, kujifunza vitu vipya, kukutana na watu wapya kwa ajili ya kesho yako.

Usikubali kuridhika na hatua ambayo umefikia sasa hivi, usikubali kuendelea kubakia kwenye hatua uliyofikia sasa. Tumia uzima ulionao kuchukua hatua ya kusonga mbele.

Kesho yako ipo mikononi mwako, kesho yako ipo kwenye uzima ambao umepewa.

Kupata huduma mbalimbali ninazotoa tembelea kwenye link hii www.jacobmushi.com/huduma

Nakutakia Kila la Kheri

Rafiki Yako

Jacob Mushi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *