Ikitokea Rais amesema vijana wote kesho tukutane nae pale Posta Dar es Salaam Atakuwa anagawa Tsh 1m ukafanyie chochote unachotaka, popote ulipo bila kujali unafanya nini bado nafasi ya kwenda utaipata. Huwezi kusema samahani naomba nije kuchukua keshokutwa, huwezi sema nitakuja jioni naomba unisubiri, huwezi kusema umepata dharura akutumie kwa mpesa.

Utakachokifanya ni kwenda na kuzichukua hizo hela. Utaahirisha kila ulichokuwa unakifanya ili tu ukazipate hizo milioni moja. Unajua ni kwanini? Jibu ni rahisi sana milioni moja ni ya muhimu sana kwako. Kwanini imekuwa ya muhimu sana? Kwasababu inaweza kutatua matatizo Fulani ambayo umekuwa nayo muda mrefu.

Hakuna atakaechelewa, inawezekana usafiri ukawa ni wa shida ghafla kwasababu ya wingi wa watu watakaokusanyika pale viwanjani.

Ukweli ni kwamba ile milioni moja ambayo kila mmoja anaweza kuifuata pale Posta kwa gharama yeyote inawezekana ikapatikana mara mia ya hiyo endapo tu ule umuhimu, utayari kutokutoa udhuru wala sababu ya aina yoyote ungeiweka kwenye ndoto na malengo yako.

Kinachofanya uairishe malengo yako ni nini? Kwanza hujayapa umuhimu, pili hujayaamini yaani bado wewe mwenyewe una wasiwasi kama ni kweli inawezekana. Kama ungekuwa na uhakika nayo kama ulivyokuwa na uhakika wa hiyo milioni basi kuna matokeo makubwa ungeyaona.

Kama ungeweza kuamka mapema hivyo kila siku kwa ajili ya ndoto zako miaka michache sana ungeshapiga hatua kubwa.

Embu yape umuhimu malengo yako, embu zipe umuhimu ndoto zako kwasababu miaka michache ijayo zitakuwa zinakupa milioni nyingi kila siku. Kwasababu miaka michache ijayo hizo shida zinazokufanya ukaifuate hiyo milioni pale posta zitakuwa zimeisha endapo ndoto yako itatimia.

Nakutakia Kila la Kheri.

Rafiki yako Jacob Mushi.

www.jacobmushi.com/coach

3 Responses

Leave a Reply to Jacob MushiCancel reply

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading