Jiunge na Mtandao Huu Uwe Unapokea makala nzuri kama hii moja kwa moja kwenye email yako

Weka email Yako hapa

Endapo itatokea umelala kisha ukaamka hukumbuki kitu chochote kuhusu wewe yaani unachoweza kufanya ni kuongea tu. Lazima utajikuta katika hali ya kujiuliza maswali mengi sana ambayo kwa haraka haraka hayatakuwa na majibu.

Swali la kwanza la muhimu utajiuliza, Mimi ni nani? Kwanini nipo Hapa? Natakiwa kufanya nini? Hutaanza kujiuliza kuhusu pesa, magari nyumba au chochote kingine Zaidi ya kutaka kujifahamu wewe kwanza. Hata ukiyaona magari huwezi kusema gari langu liko wapi kwasababu bado hata hujajua kama ulishawahi kuwepo hapa duniani. Utajaribu kukumbuka vitu mbalimbali, utawatazama watu waliokuzunguka na vitu vilivyokuzunguka labda vinaweza kukusaidia kukumbuka wewe ni nani.

Nimetaka ujaribu kuwaza hivi ili utambue vitu vya muhimu sana kwenye Maisha yako kabla ya vingine ni wewe kutambua wewe ni nani na kwa nini upo hapo ulipo. Achana na maswali nitapata wapi hela au nataka kumiliki gari, nataka kumiliki nyumba wakati bado hujajielewa wewe ni nani. Utakosea sana endapo utaanza kukimbizana na vitu ambavyo hata hujui maana yake.

Endapo utasahau kila kitu swali la muhimu na la msingi ni MIMI NI NANI? Na linalofuata ni KWANINI NIPO HAPA? Endapo ungeweza kuwa na ufahamu wa kujiuliza maswali haya wakati ule ulipozaliwa tungekuwa na dunia ya tofauti kwasababu kila mmoja angekuwa anajitambua.

Kitu cha kushukuru ni kwamba hata sasa bado una nafasi ya kujiuliza kila wakati wewe ni nani na kwanini upo hapa. Haijalishi umesahau kila kitu au unafahamu vitu vingapi. Bado una uwezo wa kujitambua wewe ni nani na kwanini upo hapa duniani.

Jiulize hili swali kama una wasiwasi na wewe. Kama unahisi inawezekana unachokifanya sio chako, unahisi labda mahali ulipo sio sahihi ulitakiwa uwe sehemu nyingine, endelea kujiuliza swali, MIMI NI NANI? Usiishie tu kujiuliza tafuta vitu ambavyo vinaweza kukupa mwongozo wa kutambua wewe ni nani. Jaribu kukumbuka vitu ambavyo vitakupa mwangaza, angali ulipokuwa mdogo ulipenda kufanya vitu gani. Jaribu kukumbuka kitu gani kilikuwa kinaleta furaha sana ndani ya moyo wako.

Utagundua tu wewe ni nani na utaacha kukimbizana na vitu ambavyo hukuzaliwa kuja kufanya hapa duniani.

Nakutakia Kila la Kheri.

Rafiki yako.

Jacob Mushi

www.jacobmushi.com/coach

4 Responses

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading