Embu jiulize leo bei ya nyama kilo moja ni Tsh elfu tano hadi elfu saba kulingana na maeneo, sasa ukipita mahali ukakuta kuna nyama ya ng’ombe safi kabisa imenona wanauza kilo moja shilingi elfu moja utavutiwa kwenda kununua? Jibu rahisi sana na ambalo kila mmoja atafanya ni HAPANA. Na itakuwa hapana kwasababu haiwezekani nyama iuzwe bei rahisi hivyo bila ya sababu.

Nyama ina thamani sana sio kitu ambacho kila mtu anaweza kukipata kama huna hela ya kutosha. Sasa kwasababu ya thamani yake ukiikuta mahali inauzwa bei rahisi sana lazima ujiulize maswali mengi ambayo hayana majibu, na pia utajaribu kutengeneza majibu yako mwenyewe kichwani, LABDA HUYO NG’OMBE WAMEMUIBA MAHALI, AU LABDA NI MG’ONJWA, AU LABDA KUNA MAMBO YA USHIRIKINA HAPO au ATAKUWA AMELALA. Kila mmoja atajiuliza swali lake na hata kama utanunua kwasababu ya usongo wa kutokula nyama kwa muda mrefu utaenda na wasiwasi sana na pia kuwauliza wengine.

Sasa embu jiulize tena kama nyama tu ambayo ilikuwa inauzwa elfu sita ikauzwa elfu moja ghafla itakupa wasiwasi wakununua inakuaje unataka kupata mafanikio kirahisi? Iweje utegemea mafanikio makubwa yaje kama maji yanayotiririka kutoka mlimani?

Kwanini sasa ukikutana na changamoto unaogopa na kusema hutaki tena? Ina maana umeshindwa kutambua kwamba mafanikio makubwa ni kitu cha thamani sana na gharama zake ni changamoto ambazo unapitia?

Naomba utambue Rafiki kwamba kama wataka mafanikio makubwa lazima ukubaliane na gharama zake. Kama wataka kuitwa mtu mkuu lazima ukubali kudharaulika, hiyo ndio gharama ambayo wapaswa kulipia. Ukiona hakuna gharama yeyote hicho kitu kinaweza kuja kukusumbua. Ukiona nyama inauzwa bei rahisi sana mtaani inaweza kuja kukuletea ugonjwa endapo utakimbilia kwasababu ya bei rahisi.

Jipe nafasi ya kutambua gharama unayopaswa kulipa na ulipie kikamilifu. Usiogope, usione mbona mambo ni mengi sana, usione mbona kuna ugumu sana, hizo ndio gharama, wewe zilipe tu baada ya muda utaanza kufurahia utamu wa kile ulichokuwa unakilipia.

Nakutakia kila la Kheri.

Ubarikiwe sana.

Rafiki Yako

Jacob Mushi

www.jacobmushi.com/coach

4 Responses

  1. Asante kaka kwa kunijenga na kunipa go ahead maana kuna wakati unapitia unakata tamaa lkn kwa somo hili kuna kitu kikubwa nimejifunza, ubarikiwe sana

Leave a Reply to Felista kazondaCancel reply

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading