Ni mara ngapi umewahi kuambiwa kuhusu wengine, mfano; “Nilimwona Fulani akiingia Gesti Jana”, “Fulani ana Mwanamke Mpya” na mengine mengi. Ukweli ni kwamba huenda umeyasikia sana kutoka kwa watu au hata wewe ulishawahi kumwambia mtu.

Sasa nikwambie kitu kimoja, hayo ni maoni tu ya watu ambayo hayana ukweli halisia. Ngoja nikupe kisa hiki, Miaka michache iliyopita nilikuwa na Rafiki yangu mmoja wa kike ambaye alikuwa anasoma chuo cha SAUT MWANZA. Sasa binti huyu alikuwa anapendwa sana na baba yake na hivyo mara kwa mara baba akipita Mwanza kwa ajili ya kazi zake lazima wakutane wale na waongee. Mara zote baba akija hushukia Lodge iliyopo karibu na chuo kwa binti ili iwe rahisi kukutana na kula pamoja.

Sasa huyu Binti ilitokea mahusiano yake yalivunjika kwasababu tu kuna mtu alimuona akishuka kwenye bodaboda halafu akaingia lodge alipo baba yake. kwa sentensi moja tu, “Nilimwona Akiingia Gesti Jana Jioni” kila kitu kikaharibika.

Sasa kikawaida ukiwa chuo unaweza kujulikana na watu wengi lakini wewe ukawa na marafiki wachache, na hawa wachache ndio watajua mambo yako. Hawa ndio utawaambia ukiwa umetoka kwenda kukutana na baba yako, au hata kwenye mambo mengine. Sasa endapo tu wale ambao wanakufahamu lakini hawakujui vizuri wanaweza kukuona ukiwa unaingia lodge, kwa haraka haraka kitakachokuja kwenye akili zao ni kwamba umeenda kukutana na mwanaume wako au umeenda kufanya umalaya.

Sasa hawa wakija kukutana na marafiki zao wanaweza kueneza maneno hayo kwamba wewe unamsaliti mpenzi wako mara kwa mara kwasababu wanakuonaga ukiingia lodge. Lakini huo sio ukweli wewe huwa unaingia lodge kuonana na baba yako mzazi. Na sio kwamba hata mnaonania chumbani ni kwenye restaurant tu ya palepale lodge. Lakini wale wasiokujua vizuri walikuona kwa getini na tayari wakaanza kutoa hukumu zao.

Kwa kupitia maneno tu ya mtu aliekuona ukiwa getini unaingia lodge yanaweza kuvuja mahusiano yako. Mfano siku hiyo uliondoka bila kumuaga mpenzi wako kwasababu labda ilitokea tu dharura baba amekuja ghafla na anaondoka jioni hiyo hiyo. Mpenzi wako akaja kusikia umeonekana unaingia lodge mida ya jioni, hata ukijaribu kumueleza hatokaa akuelewe na mnaweza kuvunja mahusiano.

Nataka niongee na Watu Wawili Hapa:

Wewe unaependa kuzungumza Maisha ya watu kwa vitu ambavyo huna uthibitisho navyo, nataka nikwambie tafuta mambo ya muhimu ya kufanya kwenye Maisha yako. Achana na Maisha ya watu, kwa maneno yako tu machache unaweza kuvunja mahusiano ya watu. Kwa maneno yako yasiyo na uthibitisho wa kutosha unaweza kuwavurugia Maisha wenzako.

Achana na Maisha ya wengine fanyia kazi Maisha yako, wewe mwenyewe una matatizo kibao yanakusonga achana na ya wengine kwasababu haulipwi chochote hapo.

Wewe ambayo unapokea maneno ya kusikia, nataka nikwambie maneno yoyote unayosikia kuhusu mtu kutoka kwa mtu mwingine mara nyingi hayana uhalisia. Mara nyingi mtu anaongezeaga kile anachoamini yeye kuwa ni kweli. Mtu akikuambia alimuona Fulani akiingia lodge Usiishie kujawa na hasira bila kujua vitu vyote vya muhimu. Tumia akili zako vizuri, usikimbilie kumhukumu mtu kwa maneno ya kusikia.

Nakutakia Kila la Kheri.

Rafiki Yako Jacob Mushi.

www.jacobmushi.com/coach

7 Responses

Leave a Reply to Peter mahunjaCancel reply

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading