Kila mmoja ana kitu ambacho amezaliwa kukifanya hapa duniani. Inawezekana bado hujatambua kusudi la wewe kuwepo hapa duniani.  Ni muhimu sana kutambua.
Simamia nafasi ya kwa bidii na kwa ubora wa hali ya juu.
Upo kwa ajili ya kuonya, onya kwa bidii.
Upo kwa ajili ya kufundisha,  fundisha kwa bidii bila kuchoka.
Umeletwa duniani ili uimbe,  imba sana bila kukata tamaa.
Wewe unawaongoza wengine, simamia nafasi yako vyema.

Fanya kile ulichoitiwa hapa duniani ipo siku utaulizwa.  Usipoteze muda kufanya yasiyo kuhusu. Tumia fursa zinakuja mbele yako kwa bidii ili utimize kile unachokisimamia.

Nikutakie Siku njema.

Jacob Mushi
Entrepreneur & Author.
Blog: www.jacobmushi.com
Email: jacob@jacobmushi.com
Phone: +255654726668

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading