Hongera sana kwa kuona mwaka mpya, nafurahi pia kuona umesoma Makala hii kwa mara ya kwanza kwa mwaka 2019. Nimekuwa nahudhuria mikesha na matamasha ya kuingia mwaka mpya na siku zote nimekuwa najifunza kitu ambacho kimekuwa kinajirudia sana. Hakuna mwaka ambao umewahi kutabiriwa mabaya, na hata kama watasema utakuwa mwaka wenye magumu lazima watayataja mazuri mengi yatakuja.

Ukweli unakuja kwamba ili mwaka uwe wa ushindi, mavuno, kuvuna, kuinuka, kusogea, kufika viwango vingine inakupasa wewe binafsi uweke juhudi za kipekee na tofauti. Lazima wewe binafsi ujipange na ukubali kujitoa vya kutosha.

Mabadiliko na maendeleo yako sio muujiza, hakuna mafanikio ya kimiujiza Rafiki yangu. Hakuna mahali utakwenda kupewa nguvu Fulani ambayo itakufanya kila unachokifanya kifanikiwe vile unavyotaka. Acha kabisa kupoteza muda wako mwaka huu kwenda sehemu hizo za kupewa nguvu za namna hiyo.

Kila mmoja anaanza mwaka kwa hamasa kubwa na kelele nyingi lakini baada ya siku chache utaanza kuona kila mmoja analalamika kwamba Maisha ni magumu, mwezi huu haufai na mengine mengi. Baada ya muda sio mrefu sana utaanza kusahau kabisa malengo uliyojiwekea mwaka huu, pia inawezekana mpaka sasa hujaweka malengo yeyote na unasubiria mambo yatokee yenyewe.

Utakuwa unaendelea kupoteza muda wako kama mpaka sasa hujajua ni vitu gani unataka kwenye mwaka huu. Unajinyima haki zako wewe mwenyewe, unajikosesha fursa wewe mwenyewe, unajiweka kwenye hali mbaya wewe mwenyewe.

Habari njema ni kwamba bado nafasi ipo kama mpaka sasa hujaweka malengo yeyote anza leo andika kila kitu unachotaka kitokee kwenye Maisha yako mwaka huu. Andika pia ni lini unataka vitokee vitu hivyo na ni vitu gani unatakiwa ufanye ili viweze kutokea kama unavyopanga.

Kipaumbele chako kikubwa kwa mwaka huu kiwe ni wewe kuwa bora Zaidi hii ni kwasababu ukiwa bora Zaidi basi na sehemu nyingi kwenye Maisha yako zitakuwa bora. Hakuna kinacholeta matokeo mabaya kwenye Maisha yako tofauti na wewe ambaye sio bora. Ukiwa bora utapata matokeo bora, ukiwa mbovu utapata matokeo mabovu.

Tumia nguvu nyingi katika kujiboresha kuliko hata unavyowekeza kwenye vitu vingine hii ni kwasababu wewe usipokuwa bora hata hivyo vitu vingine hutaweza kuvisimamia. Ukitaka kumaliza mwaka vizuri na matokeo chanya hakikisha wewe unakuwa bora Zaidi.

Mwisho ni kwamba kama unataka matokeo anza sasa, usiseme tena mpaka tarehe fulani au ngoja mpaka mwezi huu ufike katikati. utachelewa sana chukua hatua sasa rafiki yangu.

Karibu kwenye program ya mwaka wa ushindi kama utahitaji msaada Zaidi katika kuwa na mwaka wenye matokeo chanya na mwaka wa mtu alie bora Zaidi. Bonyeza maneno haya

Jiunge na Mtandao wetu uwe unapokea makala hizi moja kwa moja kwenye email yako. Mwishoni mwa makala hii kuna sehemu ya kuweka email na chini yake pameandikwa Subsrcibe. Weka email kisha Bonyeza Subscribe.

Ubarikiwe sana,

Rafiki Yako, Kocha Jacob Mushi

www.jacobmushi.com/kocha

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading