Miaka kama 10 iliyopita Kulikuwa na bibi mmoja kijijini kwetu alikuwa anauza maziwa fresh.
Maziwa yake yalikuwa ni matamu sana na pia masafi hivyo kusababisha watu wengi kuyapenda na kuyasemea vizuri.

Kadiri watu walivyoyasemea vizuri ilifika wale waliokuwa wanauza maziwa kama yeye ikabidi wafunge kwa kukosa wateja. Watu Karibu mtaa mzima ulihamia kwake.

Bibi yule alizidiwa na wateja. Kiasi cha maziwa alichokuwa anatoa kilikuwa kidogo kulinganisha na idadi ya wateja.

Ikabidi bibi huyu aazimie jambo moja. Alianza kuchanganya maziwa yake na maji.

Kidogo kidogo maziwa yalianza kutosha lakini yakaanza kupungua ubora. Wateja wakashtukia mmoja akaanza kuwaelezea wengine na Habari zikasambaa kwamba maziwa yanachanganywa na maji.

Tabia ile ikampotezea bibj yule wateja. Mmoja mmoja Wakaanza kupungua. Ikafika wakati akawa hauzi kabisa.

Bahati mbaya Hakujua wateja walimkimbia kwasababu ya kuchanganya na maji maziwa yake. Aliamini amelogwa.

Bibi akaanza kuwachukia wale wauzaji wenzake kwani walianza kufungua upya biashara zao na wateja wakahamia kwao.

Bibi akaamua kwenda kwa mganga kutafuta dawa. Kumbe ndio anaharibu kabisa, badala ya kupata dawa akajikuta ameua na ng’ombe zake zote kwa dawa za mganga.

Unajifunza nini?

Njia pekee ya wewe kuendelea kuhudumia watu wengi ni kutokukubali kushusha viwango vyako.

Ni Bora uhudumie watu wachache kwa ubora kuliko watu wengi kwa ubovu.

Ni Bora uongeze bei kuliko kupunguza viwango.

Hata mahindi hupanda bei pale yanapohitajika sana.

Kubali kwamba changamoto unazopitia wakati mwingine ni wewe umezisababisha.

Achana na imani za kishirikina hazina msaada wowote kwenye biashara yako.

Rafiki Yangu naamini Umejifunza kitu kikubwa.

Makala Hii Imeandikwa Na Jacob Mushi, Mwandishi na Mjasiriamali.

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading