Nilimpenda sana, nilimwonesha mapenzi yote, nilimpa kila alichokuwa anataka lakini nimeambulia kuachwa. Hayo ni mojawapo ya maneno ambayo watu wengi wamekuwa wakiyatoa baada ya kuchwa na wale waliokuwa wanawapenda sana.

Nimetafakari nikajakugundua kama ni kweli ulikuwa unamfanyia mambo yote mazuri na kumpa kila alichokuwa anataka halafu akaja akakubwaga ukweli ni kwamba sio wewe uliepoteza bali yeye ndie aliepoteza mtu aliekuwa anampenda sana. Ukiweza kuubadilisha huo mtazamo unaokufanya uendelee kuumia utapona maumivu uliyonayo.

Kikubwa hapa sio wewe kumpenda sana, wala kumpa kila alichokuwa anataka kikubwa hapa ni wewe ulipokuwa unajitahidi kuwa mtu sahihi kwake halafu akakuacha. Kwako hakitapungua kitu bali kwake ndio kutapungua kwasababu alikuwa anapokea upendo hataendelea kupokea tena kutoka kwako.

Nataka ubadili mtazamo wako ili usiendelee kuumia wala kuwaza kupoteza. Unapoumwagilia maji mti na kuutunza kwa gharama kubwa halafu ukaja kunyauka na kupotea hupaswi kuuchukia ule mti, utaumia kwa muda kidogo kwasababu ya ule upendo ulikuwa nao juu ya mti halafu utajaribu tena kupanda mti wa aina nyingine.

Usiweke mtazamo wa kupoteza kitu cha maana sana kwako wakati mtu huyo hakujali yale ambayo ulikuw unamfanyia. Ni kweli kuumia kupo na lazima uumie kama ulikuwa unapenda kweli ila hupaswi kuendelea kuumia milele, hupaswi kuendelea na mamumivu Maisha yako yote.

Usikubali kudumu na maumivu ndani ya moyo wako juu ya mtu yeyote aliendoka maishani mwako. Hakuna kinachodumu milele, sisi wenyewe hatudumu ipo siku tunakufa, watu pia hawadumu ndani ya Maisha yetu. Ukiona mtu ameondoka ujue basi ndio wakati wake wa kuondoka umefika.

Nakutakia Kila la Kheri.

Rafiki Yako Jacob Mushi.

#usiishienjiani.

www.jacobmushi.com/coach

9 Responses

  1. Nimekuelewa sana tena sana kiongozi hili wazo sikuwahi kuliwaza ila nilivyolipokea naamini litaponya na kufungua wengi kutoka kwenye matatizo kama haya.

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading