#SIRI_7
Siku moja nilijiuliza swali Nikiweza kutimiza ndoto yangu ya gari aina ya BMW X6 baada ya hapo nikaambiwa nimebakiza masaa machache nife  nitafurahia?

Nikajiuliza tena Nikiweza kutimiza ndoto yangu ya kujenga nyumba nzuri sana ya kuishi halafu nikaambiwa  bado siku mbili ufe je nitafurahia?
Nikasema tena na moyo Nikitimiza ndoto yangu ya kumuoa mke mzuri sana imetimia halafu nikaondoshwa duniani je nitafurahia?
Nikapata jibu kwamba yote hayo ukiyatimiza huwezi kuanza kufurahia ukifa bali utajuta.

Umeteseka sana miaka mingu ili ndoto yako itimie ya kumiliki vitu vizuri halafu unaondoka bila kuvifaidi.
Nikasema muda wangu hapa duniani nitautumia kufanya vitu ambavyo hata nikiondoka kesho nitaviacha bado vinaishi.
Kuwa na ndoto ya kumiliki gari zuri sio vibaya,  nyumba nzuri, kuoa au kuolewa sio vibaya. Ubaya unakuja pale ambapo hayo ndio mambo makuu kwenye maisha yako.  Huna jambo jingine unalolipigania libaki duniani.
Embu jiulize aliegundua mtandao unaotumia kusoma huu ujumbe yeye nyumba kwake ni nini? Gari nini? Anasa yeyote unayoijua wewe kwake ni ya gharama?
Hivyo vyote kwake ni vitu vidogo sana kwasababu aliwekeza kwenye kitu ambacho kinabaki daima. Hata akiondoka leo alichokianzisha kinabaki.
Kama ndoto yako kubwa sana ni kwa ajili yako mwenyewe hiyo ni ndoto ndogo sana.
JIPATIE NAKALA YA KITABU CHA
#SIRI_7_ZA_KUWA_HAI_LEO
Jacob Mushi
www.jacobmushi.com
0654726668

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading