Watu waliofanikiwa wanaendelea kufanikiwa kwasababu wapo tayari kufanya hata yale ambayo hawajisikii kufanya. Unajua kuna vitu unatakiwa kuvifanya halafu mwili unakuwa umechoka hivi unasema nitafanya kesho au siku nyingine.

Kuna wakati unakuwa umechoka sana hadi yale mambo ya muhimu unataka kuahirisha, unatakiwa ujue kwamba kitu pekee ambacho hutakaa ukipate tena ni muda. Lazima ukubali kujitoa vya kutosha ili ufanikiwe.

Sisemi kwamba unapaswa kujiumiza hapana ila unatakiwa ulipe zile gharama ambazo zinastahili kile unachokitaka. Wewe umeenda Dukani una elfu kumi halafu unataka kununua kitu cha elfu ishirini kamwe huwezi kupata hata ukilia. Njia pekee ya kupata ni wewe kuongeza pesa, hivyo hivyo na mafanikio sio kama bahati kwamba utafika tu hata usipo weka juhudi.

Lazima ujue ni yapi unapaswa kufanya ili kupata kile unachokitaka. Kuna nyakati itabidi hata usielewane na wale unaowapenda kwasababu na wao wanaweza kuwa sababu ya wewe kukosa kile unachokitaka. Kuna wakati itabidi was ahau kidogo zile simu ambazo umekuwa unawapigia mara kwa mara kwasababu umeweka lengo na unataka litimie.

Usipokuwa tayari kulipa gharama, sahau kuhusu mafanikio. Mafanikio sio lelema, sio bahati ambayo kama ipo utakutana nayo Njiani. Mafanikio ni kujitoa, kufanya vitu vya tofauti na wengine. Kufanya vitu ambavyo wengi wanaogopa kufanya.

Ukiamua na ukawa tayari kufanya hata yale ambayo unajisikia uvivu na kuchoka basi utaweza kufika sehemu ambazo wewe hujawahi kufika. Ukiamua kuzungumza na watu ambao ulikuwa unaogopa na ukawasumbua utajikuta unapata kile ambacho unakitaka. Hakuna kitu chenye thamani kinachopatikana kwa urahisi.

Kama dhahabu ingelikuwa inaweza kuchimbwa na kila mtu wala isingeuzwa ghali, embu tazama wale ambao unazama chini kabisa kuifata dhahabu, wengine hupoteza Maisha humo kwasababu dhahabu ina thamani kubwa sana. Kile unachokitaka kama haupo tayari kujitoa vya kutosha huwezi kupata matokeo unayotaka.

 

Ubarikiwe sana,

Rafiki Yako, Jacob Mushi

www.jacobmushi.com/huduma

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading