Penda kuwaweka wengine mbele kwanza ndio utaweza kufurahia kile unachokifanya. Unataka kununua gari, Sema napambana ninunue gari ili niwahamasishe wengine kuwa inawezekana ” Chochote kile unachokifanya hata kama ni wewe unafaidi jaribu kuweka katika namna ambayo wengine wanaguswa pia.

Furaha ya kweli haipo katika vitu tunavyomiliki ila katika watu tunaowasaidia.

Furaha ya kweli ipo katika kuwasadia wengine, na ni kwamba umezaliwa una kila kitu ndani yako kwa ajili ya kuwasaidia wengine. Biashara unayoifanya sio kwa ajili yako ni kwa wengine, inawezekana ni Watoto wako, Wateja, na hata watu ambao huwajui.

Ukitaka kusahaulika haraka hapa duniani ni kuwa mbinafsi, kuangalia Zaidi kile unachokipata kuliko thamani unayotoa kwa ajili ya wengine. Waweke wengine mbele kwanza na chochote unachokifanya kama hakimgusi mtu basi usikifanye.

Niko Njiani natembea nikawa nawaza kwamba kuna mtu kafungua Bookshop anauza vitabu ambavyo viliandikwa karibia miaka 100 iliyopita. Hawa waandishi hawana undugu na huyu muuzaji, lakini kwa kupitia kazi iliyofanyika miaka 100 iliyopita kuna mtu anapata pesa ya kula, ada ya watoto na kadhalika.

Nikawaza na kusema hivi hawa waandishi wangesema “naandika Kitabu cha nini wakati nitakufa na kuviacha,” naandika Kitabu cha nini wakati sina shida yoyote, naweza kula, nina nyumba nzuri sasa vitabu vya kazi gani”. Ila kwasababu walijua hawaandiki ili wapate hela ya kula kwa wakati huo, na hata kama wangepata kulikuwa hakuna shida. Wamefanya kazi yao wameondoka duniani wameacha watu wengi wakiendelea Kufaidika na kazi waliyoifanya.

Embu fikiria unachokifanya sasa hivi ni kwa ajili yako au kwa ajili ya wengine? Endapo ikatokea ukaondoka sasa hivi unachokifanya kitaendelea kuwa baraka kwa wengine?

Ubarikiwe sana,

Rafiki Yako, Jacob Mushi

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading