Ni muhimu sana uweze kujisikiliza na kutambua moyo wako unakwambia nini.
Moja ya vitu ambavyo tunakwama ni kushindwa kujisikiliza sisi wenyewe.

Unaweza kuwasilikiza wengine lakini huwezi kujisikiliza wewe unataka nini.

Mara nyingi ili. Uweze kujua kile unachokifanya kama ni kweli ni kusudi lako ni kuanza kusikiliza unajisikiaje unapofanya.
Kama unajisikiaje furaha fulani ambayo haielezeki ndani yako maana yake kile unachokifanya ndio umezaliwa kuja kufanya.

Kama kazi unayofanya wewe hujisikii hamasa yeyote hadi tarehe za mshahara zifike kuna tatizo.
Kama biashara yako unachojali zaidi ni faida unayopata kuliko watu wanavyosaidika maana yake hicho sio kitu chako.

Kabla ya vitu vyote cha kwanza kupimia kazi yako ni moyo wako na sio pesa. Ili mtu aweze kufanya kazi kwa bidii kwanza ni lazima aanze kuipenda kazi na kwa kuipenda kazi Ataweza kufanya kwa bidii kiasi ambacho kitaweza kumlipa.

Huwezi kupanga mipango mikubwa kwenye kitu ambacho hakileti furaha moyoni mwako. Siku zote mtu anaetaka Kudumu na wewe unamsikiliza anachokiongea. Ukiona mtu anasema tunasogeza sogeza tu maisha hapa ujue anachokifanya hakipendi.

Anza kupenda au acha katafute unachokipenda ufanye. Hapo utaweza kutengeneza matokeo makubwa sana.

Nakutakia Kila la Kheri.
Ubarikiwe sana.
Rafiki Yako Jacob Mushi.
www.jacobmushi.com/coach

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading