“A creative man is motivated by the desire to achieve, not by the desire to beat others.” -Ayn Rand
Mtu mbunifu anahamasishwa na Kutimiza kile alichokipanga na sio kuwashinda wengine.Lengo lako lisiwe kuwa bora kuliko wengine kwasababu tayari wewe una kitu cha pekee sana ndani yako ambacho wengine hawana.
Huhitaji kushindana na wengine unahitaji kushindana na malengo yako. Uwe bora kuliko jana na sio kuliko wengine.
Kile Mungu alichoweka ndani yako ndio upambane kukitimiza na sio kupambana kuwapita wengine.
Nakutakia Kila la Kheri.
Ubarikiwe sana.
Rafiki Yako Jacob Mushi.