Badala ya kubadilisha aina ya maisha unayoishi baada ya kuongezeka kwa kipato Wekeza zaidi kwanza.

Badala ya kukununua vitu ambavyo vitakuongezea matumizi ya pesa zaidi nunua vitu ambavyo vitakurahisishia kupata pesa zaidi.

Badala ya kuongeza wanawake wengi Wekeza Kwenye baadae ya watoto wako.

Badala ya kutaka kila mtu ajue umepata pesa weka nguvu kubwa zaidi katika kuwainua wale ambao unaowapenda na kuwajali.

Haitakusadia chochote kupandisha aina ya maisha yako kwa haraka baada ya kiwango chako cha pesa kuongezeka bali kutakuangusha.

Unajua kabisa kuna aina ya Tv ukinunua lazima itakubidi Ubadili hata masofa uliyonayo ili viendane. Na kun sofa ukinunua itakubidi hata ile kapeti uliyoizoea ya kawaida uibadii. Vivyo hivyo hata kabati lile litatakiwa libadilishwe kwasababu haliendani na sofa n TV.

Mwisho wa siku unajikuta maisha yako yameishia kubadilisha vitu na hakuna cha maana ulichofanya siku chache za mbele utaanza kuona tena zile pesa hazitoshi. Kumbe ungewekeza, kumbe ungewaza kuizalisha zaidi ingekuwa na manufaa zaidi kwako.

Ni rahisi mtu kutamani simu ya gharama wakati huo huo hana biashara yoyote anayofanya.
Mtu Mmoja akasema kama huku duniani ungekuwa peke yako, vitu vingi sana hata vingepatikana bure usingevichukua. Kuna nguo wala zisingekutamanisha kuvaa.

Vitu vingi ulivyonavyo ulinunua kwasababu unataka watu wakuone. Ukweli ni kwamba hao unaotaka kuwaridhisha hawakusaidii chochote. Hao unaotaka waone umependeza hata hawakufikirii.

Sio kwamba usinunue chochote cha gharama la hasha, unaweza kuwa na malengo hayo lakini hakikisha unazo fedha za kutosha. Usiniambie fedha hazitoshagi, huo ni msemo wa maskini pekee. Matajiri wanajua fedha zinatosha matumizi yeyote wanayoyataka kwasababu kuna nyakati walisahau vitu vizuri kwa ajili ya baadae.

Mtu yeyote anaekushauri kuwa utafute halafu utumie yote kwasababu hujui utakufa lini huyo amekosa matumaini na wala usimsikilize. Mimi nakwambie tafuta na tumia kwa makini huku ukiwekeza zaidi na kuzalisha zaidi kwa ajili ya baadae. Pia sio lazima kila unachokitafuta sasa hivi ukifaidi wewe unaweza kupanda mti ukiwa na umri wa utu uzima lakini kwa malengo ya wajukuu zako waje kufurahia matunda na kivuli. Hivyo hata kama ikatokea umeondoka kuna watu hawataishi kwa kuteseka kwasababu ya juhudi ulizoweka wewe.

Maisha Yako ni Maamuzi Yako.

Rafiki Yako, Kocha Jacob Mushi.

www.jacobmushi.com/coach

8 Responses

Leave a Reply to MichaelCancel reply

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading