Kinachoangusha mtu sio shoka moja lilipigwa kwa nguvu bali ni mkusanyiko wa kukatwa kidogo kidogo hadi mti unafikia hatua unakuwa umeanguka. Yale mambo makubwa unayotaka kuyafanya kwenye maisha yako unaweza kuyatimiza tu endapo utaamua kuanza kwa hatua ndogo ndogo.

Angalia ni kitu gani kidogo tu ambacho unaweza kufanya na kisha ukifanye. Usikae na kusema sina mtaji wa kutosha lakini kile kidogo ulichonacho hujaweza kukitumia. Kabla hujataka kuifikia kumi basi hakikisha umeweza kuitumia tano vizuri.

Kuna hatua hutaweza kuzifikiwa kama muujiza lazima uweke nguvu kidogo kidogo kila siku. Miaka mitano iliyopita ulikuwa unalalamika tatizo sina mtaji lakini ungeacha kulalamika na kuanza kuchukua hatua hata ya kuweka pesa kidogo kidogo kila siku au kila mwezi mwaka huu ungekuwa umefika hatua nyingine.

Rafiki nataka nikwambie chochote kikubwa unachotaka kufanya usitake kukianza kikubwa tafuta namna unavyoweza kuanza kidogo kwa hatua ndogo. Hii itakusaidia sana kukuwa na pia kupata uzoefu sana tofauti ya yule ambaye ameanza moja kwa moja akiwa na kila kitu.

Pata vitabu Vyangu kwa kubonyeza link hii www.jacobmushi.com/vitabu

Nikutakie Kila la Kheri.

Rafiki yako

Jacob Mushi.

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading