Miaka michache iliyopita kuna vingi vilivyogunduliwa kipindi hiki havikuwepo kabisa na vingine hata havikudhaniwa kama vingewezekana. Kilichofanya haya mambo makubwa tuyaonayo sasa yaweze kutimia ni kile kitendo cha watu kutaka kujua wanawezaje kuleta suluhisho kwenye jamii.

Ni muhimu sana kama unataka kuwa mmoja wa watu ambao wataleta mabadiliko kwenye dunia hii basi uweze kujiuliza swali hili,Ni kitu gani kitafuata baada ya hiki? Kwasababu hata hivi vilivyogunduliwa havitadumu milele.

Ukiweza kuwa na majibu ya ni nini kifuatacho kwenye fursa mbalimbali wewe utakuwa mtu pekee ambaye anakwenda mbele zaidi ya mawazo ya wengine na kuleta mabadiliko. Inwezekana, chochote kile ambacho umeweza kukiwaza kwenye akili yako kinawezekana kufanyika na kikawa halisi.

Usiogope Kuwa mtu wa kuchukua Hatua,

Kuwa mtu mwenye uvumilivu,

Kuwa mtu ambaye anajifunza mara kwa mara,

Kuwa mtu ambaye anajiuliza maswali mengi na kuyatafutia majibu.

Usiwe mtu mwenye tamaa ya mafanikio ya haraka.

Usiwe mtu ambaye anataka kuona wengine wanaumia ili tu yeye atomize kile anachoona kinafaa.

Usiwe mtu asiejali binadamu wengine (Hii itakusaidia usije kutengeneza vitu ambavyo vinaweza kuangamiza wanadamu).

Yapo mengi ambayo ningeweza kukwambia, Usipoteze Imani yako kwamba inawezekana, pamoja kwamba wapo wengi watashindwa kuona vile unavyoona wewe hiyo sio sababu ya wewe kuacha.

Mafanikio ni Haki Yako.

Rafiki Yako,

Jacob Mushi.

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading