503; Msikilize Mungu.

Wanadamu wana tabia ya kuongea bila kufahamu na ukifanya makossa ukawasikiliza wanaweza kukupoteza. Tukimtazama kijana Daudi aliekuwa mchunga kondoo porini, baba yake na ndugu zake walimchukulia kama mchunga kondoo, na kijana mdogo tu. Lakini Mungu mwenyewe alikuwa ameshamchagua kuwa mfalme wa Israel. Kwa akili za kibinadamu mara zote tunatazama nje. Watu wakikutazama kwa nje wanaona […]

502; Sio Kuringa, Ni Kwa Usalama Wako.

Kuna zile nyakati katika Maisha unakuwa katika kupambana huku na kule ili japo upate namna ya kuweza kuinuka na kufikia hatua Fulani ya Maisha. Sasa kuna changamoto nyingi huwa unapitia na mojawapo ni vile watu wanavyokuchukulia. Katika marafiki zako au ndugu kuna wale ambao kwenye akili zako unaanzaga kuwaweka kama ambao utawategemea hivi.  Huenda ni […]

501; Kutafuta Samaki Msituni.

Jaribu kuvuta picha upo katikati ya msitu, unatafuta samaki. Umejipanga kila kitu unacho, una chambo za kutosha, una vifaa vya kubebea na pia una hamasa na nguvu za kutosha kutafuta samaki. Kitu kimoja ambacho kitakufanya uendelee kuwatafuta samaki Maisha yako yote ni kwamba ulikuwa huna ufahamu kwamba samaki hawapatikani msituni wanapatikana majini. Haijalishi utakuwa na […]

500; Ikatokea Umesahau Kila Kitu.

Jiunge na Mtandao Huu Uwe Unapokea makala nzuri kama hii moja kwa moja kwenye email yako Weka email Yako hapa Endapo itatokea umelala kisha ukaamka hukumbuki kitu chochote kuhusu wewe yaani unachoweza kufanya ni kuongea tu. Lazima utajikuta katika hali ya kujiuliza maswali mengi sana ambayo kwa haraka haraka hayatakuwa na majibu. Swali la kwanza […]

499; Njoo Uchukue Milioni Kesho.

Ikitokea Rais amesema vijana wote kesho tukutane nae pale Posta Dar es Salaam Atakuwa anagawa Tsh 1m ukafanyie chochote unachotaka, popote ulipo bila kujali unafanya nini bado nafasi ya kwenda utaipata. Huwezi kusema samahani naomba nije kuchukua keshokutwa, huwezi sema nitakuja jioni naomba unisubiri, huwezi kusema umepata dharura akutumie kwa mpesa. Utakachokifanya ni kwenda na […]

498; Huwezi Kunizuia Tena.

Unajua hakuna kisichowezekana kwenye dunia hii endapo utakuwa umeweka nia ya dhati ya kutaka kufanikisha. Endapo utaamua kwamba hakuna chochote kinachoweza kukuzuia tena, ukikubali kila kitakachokuja mbele yako kiwe kibaya au kizuri utaamua kukitumia kama silaha ya kukusogeza mbele. Nikuambie kitu mimi sijazaliwa kwenye familia yenye nafuu ya aina yeyote, nimewahi kukosa ada ya shule, […]

497; Chuki Za Kijinga.

Unaweza ukashangaa sana kumkuta mama anawafurahia Watoto wa wengine na kucheka nao vizuri sana lakini wakati huo huo anamchukia sana mtoto alieko nyumbani kwasababu ni mtoto wa nje. Ulishawahi kukutana na mtu anakuchukia tu kwasababu wewe umefikia hatua Fulani ambayo yeye hajafika utafikiri labda wewe ndio sababu ya yeye kutokufika hapo. Ni ajabu sana kwenye […]

496; Ni Mtu Mpya Anatengenezwa.

Njia pekee ya kupata juice ya nanasi ni kulisaga na kulikamua nanasi. Kwa kawaida inaonekana kama ni kuharibu lakini ndio njia ya kupata juice. Kuna mambo yanatokea kwenye maisha kwa nje yanaonekana ni mabaya sana. Kwa nje inaonekana kama umepigwa na Mungu. Nataka nikwambie kuna kitu kipya kinakuja baada ya hayo unayopitia. Kuna bidhaa mpya […]