Mafanikio ni Mchakato.

Nilipokua sekondari tulitumia barabara mbaya sana kuelekea shuleni kitu kilichofanya safari iwe ya kuchosha sana na yenye kuchukua muda mrefu sana.Kipindi hicho barabara nzuri ya lami ilikua ikitengenezwa, kila nilipokua nikisafiri kwenda na kurudi shule nilitumia muda huo kujifunza juu ya ujenzi wa barabara! Ujenzi wa barabara unapoanza unaudhi sana kwani miti hukatwa , udongo […]

Haijalishi Umezaliwa Wapi, Maisha ni Zawadi.

Katika maisha haya kamwe usimlaumu mtu yeyote kwasababu ya kushindwa kwako au kufeli kwako jambo fulani, kwasababu kulaumu hakuibadilishi hali bali kunatengeneza tatizo lingine linaitwa KiNYoNgO. Hakuna mtu aliyetuma barua ya maombi kwa MUNGU azaliwe katika familia fulani yenye hali fulani au uzuri fulani, Wote tumezaliwa tumejikuta watoto wa fulani na fulani, Wengine wamezaliwa wamejikuta […]

531; Ni Hatua Ndogo Ndogo.

Kinachoangusha mtu sio shoka moja lilipigwa kwa nguvu bali ni mkusanyiko wa kukatwa kidogo kidogo hadi mti unafikia hatua unakuwa umeanguka. Yale mambo makubwa unayotaka kuyafanya kwenye maisha yako unaweza kuyatimiza tu endapo utaamua kuanza kwa hatua ndogo ndogo. Angalia ni kitu gani kidogo tu ambacho unaweza kufanya na kisha ukifanye. Usikae na kusema sina […]

530; Unavyovihofia Vingi Havipo Kwenye Uhalisia.

Habari ya siku rafiki, pole kwa changamoto ya Ugonjwa huu wa COVID-19. Nakutia Moyo usiogope tunakwenda kuvuka pamoja. Kila kitu hutengenezwa kuanzia kwenye akili zetu. Furaha, huzuni, matatizo, na kila aina ya vitu ambavyo hutusumbua na kutufurahisha huanzia ndani yetu. Vile unavyofikiri mara nyingi ndio huwa tatizo kuliko hata tatizo lenyewe, moyo wako ukijaa wasiwasi, […]

529; HEKIMA: Ongeza Viwango Vyako Vya Kufikiri.

Habari Rafiki yangu, leo ni siku ya pekee sana kwangu, kwani ndio siku nilizaliwa, naikumbuka hii tarehe na ninafurahi pamoja nawe. Nimekuandikia Makala hii uifurahie pamoja nami katika kukumbuka siku hii. Siku moja nilikuwa napita kwenye jingo lililokuwa linajengwa maeneo ya Mlimani City, jingo lile ni refu san ana linatamanisha. Wakati natafakari nikapata mawazo ambayo […]

527; HEKIMA: Kinyozi Anapokosea Kukunyoa.

Kinyozi anapokosea kukunyoa bila kujali amekosea kiasi gani siku zote baada ya muda Fulani nywele huota tena na utaweza kunyoa vile unavyotaka. Unapopoteza fedha haijalishi ni nyingi kiasi gani kama ni wewe mwenyewe ulizitafuta basi utaweza kuzipata tena. Unapoachwa na mpenzi ambaye ulimpenda sana bila kujali alikuwa mzuri kiasi gani, bado ipo siku utakuja kukutana […]

526; HEKIMA: Sumu Niliyowekewa Kwenye Chakula.

“Ilikuwa ni siku za mwisho wa mwaka ambapo tulikuwa na utaratibu wa kwenda kuwasalimia ndugu na jamaa ambao hatujawaona miaka mingi. Katika kuwatembelea ndugu jamaa na marafiki wengi siku moja nikapitia kwa ndugu mmoja ambaye hatukuonana muda mrefu sana. Huyu ndugu baada ya kunipokea alinisisitiza sana nile chakula. Nilimkatalia kwasababu nimepita nyumba nyingi na nimeshakula. […]

523; HEKIMA: Uzima Ni Fursa

Kuna mtu yupo hospitali anamlilia Mungu ampe uzima ulionao, halafu wewe ni mzima na unakata tamaa. Jacob Mushi Unapotaka kukata tamaa kumbuka kwamba kuna watu ambao wanalilia nguvu ulizonazo sasa hivi. Kuna mtu anaipigania pumzi ya mwisho ili angalau aendelee kuwa hai. Nataka ujue kwamba uzima ulionao ni fursa kubwa sana kwasababu ni nafasi ya […]

522; HEKIMA: Kabla Hujakata Tamaa

Jaribu Tena, ndio nasema jaribu tena bila kujalisha umeshajaribu mara ngapi. Jaribu tena ukiwa na uhakika kwamba kuna jipya ulilojifunza kichwani kwako. Jaribu tena bila ya kuhofu labda utakosea tena. Kama tayari kuna somo umepata kwenye kushindwa kwako basi utakuwa na ujasiri wa kujaribu tena. Watu wengi hukata tamaa kabla hawajakaa chini na kujitazama ni […]

SURA YA 428; Ukitegemea Hiki Pekee Utachoka Haraka.

Mwanadamu pekee aliekuwa na akili sana kuliko wanadamu wengine ni Adamu na yeye alipewa uwezo huo kwasababu alikuwa peke yake. Hivyo kwa akili na uwezo aliokuwa nao ukamuwezesha kuyaendesha Maisha yake kwa urahisi. Kwasasa kila unachotaka kukifanya kwa kiasi kikubwa kinategemea wengine, inawezekana ni vifaa, au hata watu wengine utawahitaji ili uweze kuwa na ufanisi […]