539: Ondoka Duniani Ukiwa Mtupu.

Ukishakufa ubongo wako unaoza na kila kumbukumbu iliyokuwepo humo inapotea. Chochote ulichotaka kufanya kinapotea. Chochote ambacho hukukitoa nje hakitokaa kionekane tena. Dunia itakusahau kama uliwahi kuwepo. Kule unapokwenda inawezekana ukakutana na adhabu kali sana kwasababu uliondoka hapa duniani bila kufanyia kazi kile Mungu aliweka ndani yako. Kile kilichopo ndani yako unaweza kukitoa kwa njia kuu […]

538; Jinsi ya Kuwa Mtu Bora Kila Wakati.

Habari Rafiki, Ni muda mrefu umepita bila kunisikia kwenye uwanja huu wa Makala. Ninayofuraha kukwambia leo niandaa Makala bora sana kwa ajili yako. Kinachowafanya watu waendelee kufanikiwa kwenye Maisha yao na kuwa na furaha ni pale wanapoweza kuwa bora kila wakati. Mfano kampuni ya simu ili iweze kuendelea kuuza bidhaa zake ni lazima iwe inatoa […]

537; Ingia Ndani Zaidi..

Watanzania wengi ni wavivu sana kusoma, kabla hujaamini picha ya kichwa cha habari inayosambazwa jaribu kutafuta habari nzima uisome na uelewe. Vichwa vingi vya habari huandikwa kwa namna ya kuvuta wasomaji na bahati mbaya sana wengi wenu huishia kusoma kichwa tu na kufikia hitimisho. Usiwe mwepesi pia kuamini kila kilichoandikwa kwasababu kwenye ulimwengu wa sasa […]

536: Huwezi Kuwaridhisha.

Watu wanaweza kukuchukia pasipo na sababu yoyote ya msingi. Inawezekana hata hujawahi kuwasemesha lakini wakakuchukia. Inawezekana hujawawahi kuwatendea jambo lolote lile baya au la kuudhi lakini wakakuchukia tu. Unapaswa tu kutambua kwamba hata ufanye mambo mema kiasi gani hapa duniani huwezi kupendwa na kila mtu. Huwezi kumridhisha kila mtu. Unaweza kuzungumza sentensi moja ikamsaidia mtu […]

535: Yanapokuja Usiyoyatarajia…

Weka Email Yako Hapa Upokee Makala Kama Hizi Kwenye maisha yetu ya kila siku kuna mambo mengi hutokea na kwa namna moja au nyingine mambo haya yanatuathiri moja kwa moja au kwa sehemu. Kila siku kuna mtu atakuwa amezidiwa na akakimbizwa hospitali, kuna ambaye atafiwa, kuna ambaye atapata ajali, kuna ambaye ataibiwa, kuna ambaye atapoteza […]

534: Ni Nini Kitafuata?

Miaka michache iliyopita kuna vingi vilivyogunduliwa kipindi hiki havikuwepo kabisa na vingine hata havikudhaniwa kama vingewezekana. Kilichofanya haya mambo makubwa tuyaonayo sasa yaweze kutimia ni kile kitendo cha watu kutaka kujua wanawezaje kuleta suluhisho kwenye jamii. Ni muhimu sana kama unataka kuwa mmoja wa watu ambao wataleta mabadiliko kwenye dunia hii basi uweze kujiuliza swali […]

533; Kabla Hujachukua Jiulize Ulicholeta.

Watu wengi huja kwenye Maisha yetu wakiangalia ni kitu gani watapata na ndio maana mara nyingi ukiwa huna chochote huwezi kuwa na watu wengi waliokuzunguka. Natamani wewe usiwe kama watu wa aina hii. Embu nenda kwenye Maisha ya wengine ukiwa na kitu cha kuwapa. Kila mtu ana kitu cha kutoa kwa wengine. Kinachotuzuia ni Ubinafsi. […]

532; Uliza.

Shida kubwa tuliyonayo watu wengi ni kujipa majibu ya maswali ambayo tunajiuliza wenyewe kuhusu watu wengine. Mara tu unapoingiwa na wasiwasi kichwani mwako juu ya jambo fulani usiishie kujipa majibu mara nyingi utajikuta unajipa majibu ya uongo. Unapojikuta kwenye wasiwasi wa jambo fulani ndani ya akili yako usikubali kujipa majibu mwenyewe ULIZA SWALI. Unapouliza ndio […]

531; Ni Hatua Ndogo Ndogo.

Kinachoangusha mtu sio shoka moja lilipigwa kwa nguvu bali ni mkusanyiko wa kukatwa kidogo kidogo hadi mti unafikia hatua unakuwa umeanguka. Yale mambo makubwa unayotaka kuyafanya kwenye maisha yako unaweza kuyatimiza tu endapo utaamua kuanza kwa hatua ndogo ndogo. Angalia ni kitu gani kidogo tu ambacho unaweza kufanya na kisha ukifanye. Usikae na kusema sina […]

530; Unavyovihofia Vingi Havipo Kwenye Uhalisia.

Habari ya siku rafiki, pole kwa changamoto ya Ugonjwa huu wa COVID-19. Nakutia Moyo usiogope tunakwenda kuvuka pamoja. Kila kitu hutengenezwa kuanzia kwenye akili zetu. Furaha, huzuni, matatizo, na kila aina ya vitu ambavyo hutusumbua na kutufurahisha huanzia ndani yetu. Vile unavyofikiri mara nyingi ndio huwa tatizo kuliko hata tatizo lenyewe, moyo wako ukijaa wasiwasi, […]