Habari Rafiki, Leo ni siku nyingine tena ambayo tumepewa kama zawadi kwa ajili ya kwenda kuyafanya Maisha yetu yawe bora Zaidi.

Jisemeshe Maneno Haya Kabla Hujatoka Kwenda kufanya Chochote.

“NACHUKUA HATUA, NAJIFUNZA, NAWEKA JUHUDI NA BIDII, NAVUMILIA.

MAFANIKIO NI HAKI YANGU, EEH MUNGU NIWEZESHE.”

Usidharau Kile kidogo unachokifanya. Daudi alijua kwamba anaweza kumpiga Goliath baada ya kutazama kule alipokuwa. Kujaribu kwake kupambana na dubu kulimpa nguvu kwamba hata Goliath si kitu mbele yake.

Ushindi mdogo mdogo unaopata kila siku ndio unakuonesha kuwa unaweza kufanya makubwa zaidi.

Ni ngumu kuamini unaweza linapokuja jambo kubwa, kama hujawahi kufanya jambo dogo ukapata ushindi.

Hapo hapo ulipo sasa hivi kuna vitu unaweza kuvifanya weka nguvu zako zote. Weka uwezo wako wote. Ipo siku utatumia hivyo vitu kama njia ya kupata makubwa zaidi

Ni mimi Rafiki Yako, Jacob Mushi

#UsiishieNjiani

“Piga Hatua, Timiza Ndoto Yako.”

Jipatie Vitabu vya Biashara na Mafanikio… https://jacobmushi.com/patavitabu

Tengeneza Kipato kwa kupitia Blog ….. https://jacobmushi.com/jipatieblog

Karibu Kwenye Kundi Maalumu la WhatsApp… https://jacobmushi.com/whatsapp/

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading