Kwenye dunia kila mmoja analipwa kwa thamani anayoitoa. Aina ya Maisha unayoishi ni kutokana na thamani unayoipa dunia. Mshahara unaolipwa ni thamani unayoitoa kwa bosi wako. Makossa utakayokuwa unafanya ni kusahau kwamba thamani inaongezwa, na kama inaongezwa basi ujue hiyo uliyonayo kuna kipindi itashuka kama isipoongezwa.

Yapo Mambo Ambayo unapaswa Kufanyia kazi Kila Wakati kwenye Maisha Yako.

#Kuwa Bora Kila Siku kwa Kujifunza na Kusoma Vitabu.

#Fanya Kazi Kwa Bidii Kuliko Wengine Wote.

#Hakikisha Unatoa Nguvu Zako kwenye Jambo Unalotaka Likuletee matokeo.

#Huwezi kufanya Kila Kitu Bali kuna mambo Machache Ukiyafanya Yanaleta Matokeo Makubwa. Chambua mambo ambayo mar azote ukiyafanya hukuletea matokeo makubwa na uwe unayafanya kwa bidii sana.

#Tunza Muda wako, usikubali  kutumia mitandao ya kijamii hovyo, kupoteza muda kutazama Tv, kupekua vitu visivyo na msaada kwako.

#Tenga Muda wako Na wale watu ambao unawapenda na kuwajali. Kwenye dunia ya sasa ni rahisi kuona mtu amemuweka mtu kwenye mtandao na kusema amemmiss lakini hajathubutu kumpigia simu na kuongea nae. Usikubali watu wa karibu wakose uwepo wako kwenye Maisha yao.

#Tengeneza timu ya watu ambao mna Ndoto zinazofanana na mtakuwa na umoja msikamane hadi mfikie mafanikio makubwa. Hii ndio kampani yako na mara nyingi utakuwa unapata muda wa kukaa nao Zaidi. Haina maana usiwe na aina nyingine ya marafiki lakini hawa ni watu ambao mtakuwa mnashirikishana mbinu mbalimbali za kufanikiwa kwenye kile mnachokifanya.

 

#Washirikishe wengine maarifa. Unaweza kumpa mtu zawadi ya nguo atavaa itachakaa, unaweza kumnunulia mtu chakula atakula kitaisha, lakini ukimpa mtu zawadi ya maarifa hataweza kukusahau kamwe kama atayafanyia kazi na Maisha yake yakabadilika. Njia pekee ambayo unaweza kumsaidia mtu ni kumshikirisha maarifa unayojifunza kwenye Usiishie Njiani Academy.

 

Ni mimi Rafiki Yako, Jacob Mushi

#UsiishieNjiani

“Piga Hatua, Timiza Ndoto Yako.”

Jipatie Vitabu vya Biashara na Mafanikio… https://jacobmushi.com/patavitabu

Tengeneza Kipato kwa kupitia Blog ….. https://jacobmushi.com/jipatieblog

Karibu Usiishie Njiani Academy https://jacobmushi.com/whatsapp/

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading