UNATAKA ULINZI? JUA KITU HIKI CHA MUHIMU KWENYE MAISHA YAKO.

Mwaka 2004 ulikuwa ni mwaka ambao ungeweza kuwa sababu ya wewe kutokusoma hiki ninachokiandika leo wala kufahamu kama niliwahi kuwepo kwenye ramani ya dunia hii. Lakini kwasababu ya kusudi la Mungu ambalo aliweka ndani yangu akaweza kunipa kibali nikapata tena nguvu ya kuendelea kuishi na sasa unaweza kunisikia na kusoma Makala ninazoandika. “Ilikua ni jioni […]

Jifunze Kwa Mtoto

Kuna nyakati kwenye maisha tunapitia hali ambazo zinatulazimisha kufanya mambo tusiyohitaji ila ni kwasababu tunaisikiliza mili yetu. Sio kila hali ambayo unaisikia kwenye mwili wako inahitaji kufanyiwa kazi. Ukiwa na mtoto mdogo utaweza kuniambia kwamba sio kila anacholilia mtoto unampatia. Mfano anatakiwa kulala na yeye anataka kwenda kucheza huwezi tu kumruhusu kwasababu ametaka. Anatakiwa kula chakula akalilia […]

JINSI YA KUJIJENGEA TABIA YA KUWA MSOMAJI WA VITABU KILA SIKU.

Habari za leo Rafiki yangu na msomaji wa mtandao wa USIISHIE NJIANI? Ni matumaini yangu kuwa bado hujaishia njiani kwenye safari yako ya mafanikio. Kila siku kuna hatua unapiga kutokana na yale unayojifunza hapa kila siku. Leo tunakwenda kuona ni jinsi gani ya kujijengea tabia ya kujisomea vitabu kila siku. Mojawapo ya changamoto kubwa inayowakumba […]

NILICHOJIFUNZA KWENYE MAISHA YA WENGINE MWAKA  2017. (SEHEMU YA 1)

Moja ya jukumu kubwa nililojipa kwa mwaka huu 2017 ilikuwa ni kujifunza kwenye Maisha yaw engine, na hapa ni kuona namna gani wanavyoendesha Maisha yao kuanzia ndani hadi nje. Yapo mengi sana kama binadamu unaweza kujifunza kwenye Maisha ya wenzako kwasababu tumeumbwa tofauti, tumekulia kwenye mazingira tofauti na kila mmoja ana kusudi la yeye kuwepo […]

USIRUDIE TENA AU USIJARIBU KOSA HILI MWAKA 2018

Katika Maisha tunakutana na watu ambao wanaweza kuwa baraka sana kwenye Maisha yetu hadi tukajisahau kwamba kuna siku wataondoka. Ninaposema kuondoka simaanishi kufa namaanisha kuna siku hawatakuwa pamoja nasi kama walivyokuwa nasi mwanzo. Kosa ambalo unaweza kulifanya na likasababisha uje kujuta Maisha yako yote ni kuwapa utegemezi mkubwa watu ambao hawadumu maishani mwako. Lazima ujifunze […]

Mafanikio Yanakuhitaji Uwe hivi (Binti)

Habari za Leo Rafiki na Mwanamafanikio mwenzangu. Ni matumaini yangu kwamba unaendelea vyema. Leo napenda nizungumze na mabinti ambao wanataka mafanikio. Mafanikio katika maisha na ndoa zao. Tumejifunza sana kuhusu mafanikio tukasema ni lazima uwe na Ndoto kubwa na uziandike kisha uzifanyie kazi. Pia Kwenye upande wa Mahusiano ni muhimu kuwa na Ndoto na malengo. […]

SEHEMU 2 ZA KUZINGATIA WAKATI UNATAFUTA PESA KWA BIDII.

Habari za Leo Rafiki yangu. Natumaini unaendelea vyema na kupambana pamoja na kutafuta mafanikio kwa bidii. Leo ninapenda tuangalie sehemu mbili za kuzingatia wakati tunatafuta pesa kwa bidii. Ni kweli Maisha ya sasa huwezi kuyafurahia hata kidogo kama huna pesa za kutosha. Na pesa za kutosha zinapatikana kwa kufanya kazi kwa bidii na kujifunza mambo […]

HIKI NDIO KINAKUZUIA USIFANIKIWE

Habari za leo Rafiki na mwanamafanikio mwenzangu. Ni matumaini yangu bado unapambana na hujakata tamaa. Ni muhimu sana uendelee mbele usikubali kubaki hapo ulipofikia. Kila unachokifanya kina mchango mkubwa sana katika mafanikio yako hata kama hutaona leo au kesho. Matokeo yanaweza kuonekana hata baada ya miaka kadhaa. Hivyo usife moyo wala kurudi nyuma bado safari […]

MAMBO UNAYOTAKIWA UYAPATE KWENYE MITANDAO YA KIJAMII.

Habari za Leo Rafiki na Mwanamafanikio mwenzangu. Ni furaha yangu kusikia unaendelea vyema na mapambano. Leo tunajifunza mambo matatu ya muhimu unayotakiwa uyapate ndani ya mitandao ya kijamii.  Mitandao hii imekua ni sehemu ambayo wengi wetu tunapoteza muda bila kufanya chochote cha maendeleo Kwenye maisha yetu. Ni muhimu sa ujifunze namna ya kuokoa muda wako […]

SIFA 5 ZA WATU WA KUFANYA NAO KAZI KAMA TIMU BORA YA MAFANIKIO NA USHINDI.

Mojawapo ya changamoto kubwa wanayopitia wengi sana ni kukosa timu ambayo inaweza kuwa sababu ya wao kufikia mafanikio makubwa. Kuna usemi unasema kama ndoto zako, maono yako utaweza kuyatimiza wewe peke yako basi hayo sio maono ya kutoka kwa Mungu. Vilevile kama utaweza kufanya wewe kila kitu na ndoto zikatimia basi hizo ndoto ni ndogo […]